• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mongella aipongeza ukerewe kupata hati safi

Posted on: June 5th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amepongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa kupata HATI SAFI katika Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019. Ametoa pongezi hizo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani kujadili hoja za ukaguzi kikao kilichofanyika ukumbi mkubwa wa halmashauri kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe George Nyamaha na Katibu ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri Bi Ester Chaula na Kuhudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Katibu Tawala wa Mkoa Emmanuel Tutuba pamoja na wataalamu wa ofisi yake.

Aidha Mongella amesisitiza bado kama Halmashauri mnatakiwa kuweka utaratibu wa kujadili hoja za Mkaguzi na kuwasilisha kwa mkaguzi wa nje zikiwa tayari na maoni ya kamati ya fedha pamoja na baraza ili kufunga hoja hizo.

Mongella ameitaka Halmashauri kuongeza uwezo wake wa makusanyo ya ndani na kuhakikisha fedha za asilimia 40 zinazotakiwa kwenda katika maendeleo kwani ni takwa la kisheria. Na serikali katika kuimarisha mapato ilianzisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki (POS) lakini bado kuna changamoto zilizoainishwa na mkaguzi ya wakusanya mapato kutowasilisha benki kiasi cha Tsh milioni 274, hivyo ameelekeza kamanda wa Polisi Wilaya na TAKUKURU atoa siku saba (7) fedha hizo ziwezimewasilishwa benki na taarifa hiyo iwasilishwe ofisini kwake baada ya siku saba.


Suala la madeni ya madiwani naelekeza kuwa uhakiki ufanyike kwa kushirikiana na ofisi ya RAS nay awe yamelipwa kufikia tarehe 10 juni 2020, na amesisitiza kumbukumbu zote muhimu za kuthibitisha madeni ya waheshimiwa madiwani zitumike na kukamilisha ulipaji mapema iwezekanavyo.


Mhe. George Nyamaha Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Ukerewe na diwani wa kata ya Kagunguli amewapongeza kwa namna kila diwani alivyoshiriki katika baraza hilo na kwa kuonyesha ukomavu katika kujenga hoja kwa maslahi ya wanaukerewe.


Nyamaha ameeleza namna serikali ya awamu ya tano imewezesha Ukerewe kuwa na hospitali mbili za wilaya, ujenzi wa madaraja mawili moja Bukungu na kilimabuye, fedha wa ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ikiwemo Busangumugu. “ yapo mengi mazuri ambayo Mhe Rais ametekeleza hivyo kwa niaba ya baraza hili natoa shukrani zangu za dhati”.

Aidha amewukuru madiwani wote watendaji wote kwa kufanya kazi vizuri na baraza hilo mpaka kufikia wakati huu, amewatakia heri madiwani wanapojiandaa na mchakato wa kupewa ridhaa katika vyama vyao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.