• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mongella atoa ahadi mabati 100 ujenzi wa madarasa Kisiwa cha Kweru

Posted on: February 12th, 2020


Wananchi wa kisiwa cha Kweru mto ndogo kilichopo wilayani Ukerewe wamelazimika kujenga shule ya msingi ili kunusuru maisha ya watoto wao waliokuwa wakilazimika kuvuka maji kwenda ng’ambo ya pili kuifuata elimu kwa kutumia mitumbwi.

Akizungumza wakati wa ziara Mkuu wa wilaya hiyo Mhe.Cornel Magembe alisema Shule ya Msingi Shikizi ilijengwa kwa usimamizi wa polisi hiyo, ni baada ya kuibuka kundi la watu wakidai eneo hilo kuna makabuli ya babu zao lengo likiwa ni kukwamisha harakati za ujenzi wa shule hiyo.

Alisema kipindi cha nyuma watoto walilazimika kupanda mitubwi kuifuata elimu kisiwa jirani jambo ambalo lilisababisha watoto kupata adha mbalimbali hivyo wananchi waliungana na kuweza kujenga vyumba vinne vya madarasa,ofisi moja na matundu ya choo mawili.

“Shule hii ni mradi uliogharimu Tsh 33,000,000/- ambapo inahusisha mchango wa Mkurugenzi, Mchango wa wananchi pamoja, NMB  na mifuko 193 ya saruji fedha za Mfuko wa jimbo, katika kisiwa hicho”alisema Mhe.Magembe.

Awali mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ambaye ni diwani kata ya Kanguli George Nyamaha amemweleza adhima ya wananchi wa kisiwa hiko kuwa ni kuboresha elimu na wapo tayari kukamilisha ujenzi kwa mifuko 193 iliyotolewa na Mbunge ili kupatiwa usajili hivyo wananchi wa kisiwa hicho walilazimika ujenzi wa shule kutokana na changamoto hiyo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella aliwapongeza kwa maendeleo hayo kwani kuna maeneo ambayo yanawakazi wengi lakini hawana hamasa ya kujenga shule hivyo alimuagiza Afisa Elimu wa Mkoa Michael Ligola kualakisha usajili wa shule hiyo ili kuwanusuru na adha hiyo, na kuahidi kuchangia bati mia moja ili kuunga mkono juhudi za wananchi hao.


“Kuna maeneo watu ni wengi na wanashindwa ata kujenga shule, ujenzi kwao ni ugomvi na mabishano wananchi wote wangekuwa kama wakazi wa kisiwa hiki tungekuwa mbali sana kimaendeleo na nitafuatilia madarasa mawili yaliyosalia pamoja na ujenzi wa Choo ili shule hiyo ipatiwe usajili kamili.”alisema  Mhe.Mongella.

Naye Afisa Elimu Mkoa Michael Ligola alisema Shule hiyo inatakiwa kusajiliwa ili kuwanusuru watoto hao hivyo wajitahidi kumalizia madarasa mawili na matundu ya vyoo ili kukudhi vigezo baada ya hapo watawapitisha wakaguzi na shule hiyo itasajiliwa.

Aidha wananchi wa eneo hilo wakizungumza katika mkutano wa hadhara Frank Vicent na Yusta John walisema baada ya watoto kushindwa kwenda shule unapovuma upepo ziwani wamechukua hatua hiyo ambapo hatua ya kwanza walianza na ujenzi wa shule kwa kutumia mabanzi ,wanafunzi walisoma hadi pale walipojenga shule hiyo  pia waliiomba serikali kusaidia kumaliza mapungufu yaliopo ikiwa pamoja na usajili wa shule hiyo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.