• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mradi wa Kizazi Hodari watambulishwa Mwanza

Posted on: November 21st, 2023

Mradi wa Kizazi Hodari watambulishwa Mwanza


Serikali  kupitia OR- TAMISEMI kwa kushirikiana na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Makao Makuu Arusha, limetambulisha mradi wa USAID Kizazi Hodari Mkoani Mwanza ambao umelenga kuwafikia watoto 64,266.

Akizungumza jijini Mwanza leo wakati akitambulisha mradi huo Kiongozi wa Mradi wa  USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kaskazini Mashariki, KKKT Makao Makuu Arusha, Dk. Godson Maro, amesema lengo kubwa la mradi  huo ni kuboresha afya,ustawi na ulinzi kwa watoto walio katika mazingira hatarishi na vijana walio katika maeneo ambayo yana maambukizi ya juu ya virusi vya ukimwi.

Dk.Maro amesema kwamba wanatekeleza mradi huo wa miaka mitano ulioanza Aprili Mosi ,2022 Mkoani Arusha na Kilimanjaro  kwa ufadhili wa Shirika  la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa(USAID) ambao utagharimu dola milioni 27.4 unaotarajia kukamilika Machi 31, 2027 ukiwa umewafikia walengwa katika mikoa mingine sita ambayo ni Dodoma,Singida, Manyara, Geita, Mara na Mwanza.

 “Katika Mkoa wa Mwanza mradi huu umelenga kuwafikia watoto 64,266 wanaoishi katika mazingira hatarishi ambao wameathirika au kuathiriwa na virusi vya ukimwi kwa ajili ya kuwaunganisha na huduma za tiba ambazo zitawasaidia kufubaza virusi vya ukimwi,  tunawapa elimu ya kujitambua  pamoja na huduma zingine  jumuishi,”amesema Dk. Maro na kuongeza

“Walengwa wa mradi huu ni watoto wenye umri wa miaka 0 hadi miaka 17, pia tutatambua kaya maskini zenye uhitaji na kuziunganisha kwenye vikundi mbalimbali vya maendeleo  ili viwasaidie kuongeza kipato cha kaya waweze kuwahudumia watoto wenye.

 maambukizi,”amefafanua

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka  OR-TAMISEMI Mariam Nkumbwa, ametoa rai kwa watu wote watakaohusika katika kutekeleza mradi huo kuwajibika na kufanya kazi kwa kushirikiana ili malengo ya mradi huo yatimie kwa ufasaha.

“Matarajio ya OR- Tamisemi kwenye mradi huu ni kuona matokeo yote chanya yaliyoainishwa yanatekelezwa kama kutekelezwa kama yalivyopangwa, tunaamini wakati wa utekelezaji  wa miradi huwa kuna changamoto mbalimbali zinajitokeza, tunaouzoefu kupitia miradi mbalimbali tuliyokwishaitekeleza lakini tukifanya kazi kama timu tutashirikiana ili kuzitatua,”amesisitiza.

Awali akizungumza na wadau wanaotekeleza mradi huo ofisini kwake,  Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Balandya Elikana alisema uongozi wa mkoa huo utashirikiana nao kuhakikisha kuwa malengo ya mradi yanafikiwa.

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mwanza, Faithmary Lukindo amesema mradi huo utasaidia watoto wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutokushindwa kwenda shuleni kutokana na kusumbuliwa na magonjwa nyemelezi kwa sababu watakuwa na afya nzuri kutokana na kufuata ufuasi mzuri wa dawa  pia watawasaidia kupatikana kwa vifaa saidizi pamoja na vifaa vya shuleni ili wasikose masomo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.