• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mradi wa Maji Butimba kuwanufaisha zaidi ya wakazi laki nne Mwanza

Posted on: September 8th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Chanzo Kipya cha Maji eneo la Butimba kuongeza bidii ya ujenzi ili kukamilisha kwa wakati na uweze kuwanufaisha wananchi wanaosubiri mradi huo.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo leo Septemba 08, 2022 wakati akikagua mradi mkubwa wa cha Chanzo Kipya cha Maji eneo la Butimba unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa mazingira Mwanza (MWAUWASA) huku ukijengwa na Mkandarasi Kampuni ya M/S Sogea Satom kutoka Ufaransa kwa gharama ya Tshs. 69,337,520,300 ambao ulianza kutekelezwa Februari Mosi 2021 huku ukitarajiwa kukamilika Mwezi Februari 2023.

Aidha, amesema amefurahishwa sana na Utekelezaji wa mradi huo mkubwa na amewaagiza viongozi wa wilaya ya Nyamagana kuhakikisha utakapokamilika mradi huo wa maji uliofikia asilimia 40 ya utekelezaji kuhakikisha unawanufaisha wananchi wa eneo linalozunguka mradi huo kabla ya kusambaa kwenye maeneo mengine.

Mkurugenzi wa MWAUWASA, Mhandisi Leonard Msenyera amesema mradi huo mkubwa wa kisasa umegawanyika kwenye maeneo kadhaa yakiwemo Tanki kubwa, eneo la kuondoa madini tofauti, eneo la kubadilisha tabia ya maji, chemba ya kuondoa matope, eneo maalum la kuchuja maji, eneo la kuuwa wadudu na eneo la usafirishaji na kwamba hatua hizo zithakikisha ubora na usalama wa maji kuwa wa juu.

"Mradi huu wa Ujenzi wa Chanzo kipya na kituo cha kusafisha Maji safi cha Butimba utakapokamilika kwa awamu hii ya kwanza utazalisha lita elfu 48 kwa siku hivyo utaboreshwa huduma ya upatikanaji wa maji safi kwa wakazi wapatao 450,000 katika Jiji la Mwanza kutoka Nyegezi, Mkolani, Buhongwa, Lwamina, Fumagila, Sawha, Igoma, Kishiri na Nyamanoro, aidha maeneo ya Usagara, Nyashishi na Fella katika wilaya ya Misungwi na Kisesa, Bujora na Isangijo katika Wilaya ya Magu yatanufaika pia." Mhandisi Msenyera.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.