• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mradi wa Maji kisiwani Kome-Buchosa wa Shs Bilioni 2.2 kuanza Mei mwaka huu.

Posted on: March 1st, 2023


Zaidi ya wananchi Elfu 17 kati ya elfu 58 kwenye Vijiji 8 Kisiwani Kome - Buchosa wanatarajia kunufaika na Mradi mkubwa wa Maji unaotekelezwa na Kampuni Kamba's Company Group chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini  (RUWASA) kwa zaidi ya Bilioni 2.2

Hayo yamebainishwa leo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima wakati alipotembelea Mradi huo kwenye kijiji cha Lugata na kubaini kuwa Ujenzi wa Mradi huo uliofikia asilimia 70 ya ujenzi upo kwenye hatua za mwisho za utekelezaji na kwamba ifikapo  Mei mwaka huu utaanza kutoa Maji.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema kwa kushirikiana na Wizara ya Maji atahakikisha Mkandarasi analipwa fedha zilizobaki kwa wakati na kufuatilia hatua za kupata msamaha wa kodi kwa mujibu wa mkataba wa mkandarasi huyo ili kuvitoa vifaa vilivyokwama bandarini mara moja.

Baadae Mkuu wa Mkoa alikagua maendeleo ya taaluma kwenye shule ya Sekondari ya Lugata na kusikitishwa na matokeo mabaya ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne pamoja na uwepo wa Miundombinu rafiki ya madarasa na akaagiza kukamilishwa kwa Ujenzi wa mabweni ili kuwapunguzia umbali wa kutembea wanafunzi wanapofika na kutoka shuleni hapo.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lugata, Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Erick Shigongo amesema ukamilishaji wa mradi huo utasaidia kuwaokoa akina mama wanaokamatwa na Mamba ziwani kwa kufuata Maji na kwamba suala la Magonjwa ya Tumbo kutokana na matumizi ya maji yasiyo salama itakua historia.

"Nimesikitishwa sana na maendeleo ya watoto kwenye shule hii, hatutafikia ndoto ya mafanikio kwa kufelisha watoto na ninatoa changamoto kwa walimu kutimiza wajibu na Serikali ihakikishe inatuletea walimu wa kutosha ili ujenzi wa madarasa uende sambamba ufaulu mzuri wa watoto." Amesema Mhe. Mbunge akiwa katika shule ya Sekondari ya Lugata.

Akizungumzia mradi wa Maji, Kaimu Meneja wa RUWASA Buchosa Mhandisi Elisha Sembo  amebainisha sababu za kuchelewa kwa mradi huo kwa Miezi 6 kuwa ni pamoja na kuchelewa kwa kuwasili kwa vifaa kutokana na taratibu za msamaha wa Kodi kwa vifaa vilivyonunuliwa nje ya nchi.

Naye, Ndugu Yahya Yusuph Mwenyekiti wa Kampuni ya Kamba's Company Group anesema kuwa endapo malipo ya fedha zilizobaki yatafanyika kwa wakati na kupatiwa msamaha wa kodi kwa vifaa vilivyopo bandarini mradi huo utakamilika kufikia  Mei 2023

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.