• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Bingwa tena Umitashumta Kitaifa

Posted on: June 29th, 2018

  

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima amehitimisha mashindano ya 23 ya Michezo ya UMITASHUMTA Kitaifa yaliyofanyika Mkoa wa Mwanza akimuwakilisha Waziri wa Nchi 0fisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo ambapo Mkoa wa Mwanza kwa mara ya pili mfululizo umeshika nafasi ya kwanza kitaifa.

Awali akihutubia katika kufungwa kwa mashindano hayo  Mhe.Adam Malima aliwashukuru wote waliofanikisha zoezi hilo hadi kufikia kilele juni 29 na kuwaasa  waendelee kufanikisha michezo katika shule zote Nchini.

 "Napenda kuchukua nafasi hii ya pekee kabisa kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella ambaye ndiye Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa wa Mwanza kwa uongozi wake imara uliofanikisha mashindano haya kufanyika kwa amani na usalama katika muda wote ambao mashindano haya yamefanyika," alisema Malima.

Vile vile hakusita kumpongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dokta John Pombe Magufuli kwa juhudi kubwa zakikisha  kufanikisha kuwepo kwa mashindano hayo ambayo ni fursa pekee kwa vijana hao, katika kuonyesha vipaji vyao.


Mhe. Malima aliwasisitiza wanamichezo na wadau mbalimbali wa michezo kuhakikisha wanaienzi kauli mbiu ya mwaka huu  inayosema, "Michezo Sanaa na Taaluma ni Msingi wa Maendeleo ya Mwanafunzi katika Taifa letu.”


Katika mashindano hayo Mkoa wa Mwanza umeibuka kidedea na kuwa mshindi wa kwanza kwa ujumla huku Mkoa wa Ruvuma ukishika nafasi ya mwisho Kitaifa kwa mwaka huu,ambapo  Mwanza imekuwa bingwa kwa ya pili mfululizo huku katika mchezo wa netiboli wakifanya vizuri zaidi.

Naye Mwalimu Rehema Maruzuku ambaye ndiye kocha wa netiboli aliuzungumzia Mkoa wa Mwanza kwa nafasi ya pekee.

"Kwa netiboli Mkoa wa Mwanza umeshika nafasi ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo na ninafikiri kombe hili ni la Mkoa huu moja kwa moja kwa sababu ukimiliki kombe hili kwa miaka mitatu mfululizo basi ni la kwako"alisema Maruzuku.

Kwa upande wake  mwalimu Tibu kutoka Singida hakusita kutoa maoni yake juu ya uendeshwaji mzima wa mashindano hayo.


"Mashindano ya UMITASHUMTA yameendeshwa vizuri, sema kuna baadhi tu ya Mikoa bado hawajazingatia sana suala la umri kama tumeamua kuwachezesha tu watoto wa umri fulani basi tuwalete watoto sahihi katika umri uliopangwa,"alisisitiza Mwalimu Tibu.


 Nao wanafunzi waliouwakikisha vyema Mkoa wa Mwanza hawakusita kueleza siri ya mafanikio yao iliyowawezesha kutwaa ubingwa huo ambayo ni nidhamu nzuri,kufuata maelekezo ya walimu wao na waliongeza kuwa wamejifunza vitu vingi sana huku michezo ikiwaongezea ujasiri wa kujiamini kama wana michezo, na kufanya wapate marafiki wapya na kusisitiza kuwa mwakani watafanya vizuri zaidi, ambapo mashindano hayo yatafanyika Jijini Dodoma mwakani 2019.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.