• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA INA MAZINGIRA MAZURI YA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA NA BIASHARA : RC MAKALLA

Posted on: November 24th, 2023

MWANZA INA MAZINGIRA MAZURI YA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA NA BIASHARA : RC MAKALLA


*Abainisha kuwa Mkoa unaelimisha wananchi kujihusisha na Uvuvi wa kisasa*


*Asema Mkoa huo utaendelea kuimarika na kuchangia pato la Taifa*


*Asema kuwa miradi ya kimkakati itachochea biashara na kukuza uchumi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amebainisha kuwa Mkoa huo unaendelea kuweka mazingira mazuri ya kufanya uwekezaji na biashara ili wananchi wajishughulishe na shughuli za kiuchumi na kuweza kuinua pato la mtu mmoja mmoja na Taifa.

Makalla ameyasema hayo mapema leo Novemba 24, 2023 wakati akizungumza na Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo iliyopo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Makalla amesema Mkoa huo upo kwenye zoezi kubwa la kutoa elimu kwa vijana ili waweze kujihusisha na uvuvi wa kisasa hususani kwenye vizimba jambo ambalo linahakikisha rasilimali za ziwani zinalindwa kwa manufaa ya muda mrefu.

"Kwa kuzingatia uwepo wa ziwa victoria, Mkoa wa Mwanza tunatoa elimu kwa wananchi kufanya uvuvi wa kisasa ambao ni wa kwenye vizimba na tunahamasisha wavuvi kuachana na uvuvi haramu", amefafanua.

Aidha, amebainisha kuwa uwepo wa miradi ya kimkakati inayoendelea kujengwa kama reli ya kisasa (SGR), Meli ya Kisasa ya MV Mwanza pamoja na Daraja la Kigongo-Busisi itasaidia sana kukuza biashara na kuchochea uchumi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mhe. Deodatus Mwanyika amesema kuwa pamoja na kamati hiyo kusimamia fedha zinazopelekwa kwenye miradi inahamasisha pia uwekezaji kwenye viwanda ili kuongeza thamani ya malighafi.

Ndege ya mizigo ambayo Mhe. Rais ameinunua inaweza kuwa chachu ya kufufua viwanda kwani inatoa nafasi ya kusafirisha moja kwa moja malighafi kwenda viwandani kwa hiyo Serikali inahamasisha ufugaji, kilimo na biashara za kisasa ili kupata tija.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.