• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yaadhimisha fimbo nyeupe kitaifa

Posted on: October 23rd, 2018


Chama cha wasioona Tanzania (TLB) kimesema kuwa hakina tatizo na uongozi wa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kutokana na changamoto zilizokuwa zinazokikabili chama hicho kupungua siku hadi siku.

Kauli hiyo imetolewa  jijini hapa na Mwenyekiti wa Chama cha Wasiona Tanzania Mkoa wa Mwanza Musa Mashauri  juu ya maandalizi ya maadhimisho ya fimbo nyeupe ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Mwanza.


Mashauri  amesema TLB inamshukuru Rais John Magufuli kwa upendo wa dhati kwa watu wenye ulemavu wa kutoona na walemavu wengine  nchini kwa kuwathamini na kufanya maamuzi stahiki ya kumteua mmoja wa walemavu Amon Mpanju kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

“Niseme tu sisi tunamshukuru sana Rais wetu mpendwa, anatujali na anatuthamini, nasema na mwandishi kaandike hivyo kwamba sisi hatuna shida na rais wetu kwa sasa tunampenda kwa jinsi anavyotujali,”alisema.

Akizungumzia maandalizi ya maadhimisho hayo yatakayoadhimishwa kwa kauli mbiu, “ Mafunzo ya Tehama kwa wasioona ni nyenzo jumuishi katika uchumi wa viwanda,” alisema maandalizi muhimu yamekamilika.

Alisema uamuzi wa maadhimisho hayo kitaifa kufanyika mkoani Mwanza ulifikiwa baada ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya TLB kwenye kikao chake kilichofanyika mjini Morogoro kuja na uamuzi huo.

Alisema tangu wakati huo shughuli mbalimbali za maandalizi zimekuwa zikifanyika kwa ajili ya kufanyika maadhimisho hayo, ambayo yanafanyika katika Viwanja vya Furahisha  ambayo kilele chake ni Oktoba 25 mwaka huu.

“ Mfano tuliwasilisha barua kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella kuomba mkoa wake kuwa mwenyeji wa maadhimisho haya kitaifa na alilikubali ombi letu,” alisema.

Alisema kwa msaada wa Mongella, imeundwa kamati maalum ya mkoa ya watu 20 ambayo imepewa jukumu la kuratibu maadhimisho hayo ambayo inaongozwa na Katibu Tawala Msaidizi (Miundombinu) Seif Hussein.

“ Kamati hiyo imetengeneza mpango kazi wa bajeti kwa ajili ya maadhimisho hayo, ambapo jumla ya Sh. milioni 74 zinahitajika, lakini kutokana na michango ya vifaa kwa ajili ya watu wasioona, naweza kusema tumepata karibu asilimia 80 ya lengo ”, alisema.

Aliwashukuru watu waliosaidia kufanikisha michango  hiyo ikiwemo serikali ya mkoa wa Mwanza, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Mkurugenzi wa the Desk and Chair Foundation Sibtain  Meghjee na wadau wengine wanaoshirikiana nao Mobiles Eyes Foundation Tanzania, Beta Charitable Trust, Flora  na Bilal Muslim Tanzania ambao kwa pamoja wamechangia vifaa mbalimbali vya tiba, zikiwemo fimbo nyeupe, miwani na vifaa vya upasuaji vyenye thamani ya Sh milioni 20.

“ Lakini pia kupitia maadhimisho haya, tumefanikiwa kuandaa siku ya macho, ambapo wananchi wenye matatizo ya macho watapata huduma bure ya upimaji wa macho na tumeandaa maonesho ya wajasiriamali kwa wasioona lengo likiwa ni kuionyesha jamii kuwa wasioona sio ombaomba na wao wanaweza kufanya kazi na kujipatia kipato,” alifafanua.

Alisema kutokana na ufinyu huo wa bajeti, baadhi ya shughuli ambazo zilipangwa kufanyika kwenye maadhimisho hayo zimeondolewa. Alizitaja shughuli hizo zilizoondolewa kuwa ni upandaji wa miti 400 kwa ofisi za wakuu wa wilaya za Nyamagana na Ilemela, Shule Maalum ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi ya Mtindo iliyoko wilayani Misungwi.


Akikabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Philis Nyimbi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkurugenzi wa the Desk and Chair Foundation Sibtain Meghjee alisema wametoa vifaa hivyo kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali za kuwasaidia watu wenye ulemavu nchini.  

Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt.Philis Nyimbi aliishukuru taasisi ya the Desk and Chair Foundation kwa moyo wako wa upendo wa kuwajali watu wenye ulemavu na mahitaji yao na kuyaomba mashirika na wadau wengine wa maendeleo kuiga mfano wao.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa (RMO) Dkt.Silas Wambura akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo, alithibitisha kuwa vifaa hivyo vinafaa kwa huduma za utoaji wa tiba na kinga kwa jamii ya watu wasiiona nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi hayo Seif Hussein alisema maandalizi kwa ajili ya maadhimisho hayo yamekamilika na kwamba Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ni Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia ulemavu Mhe.Stela Ikupa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.