• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA YAADHIMISHA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Posted on: April 26th, 2024

MWANZA YAADHIMISHA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


Mkoa wa Mwanza leo umeadhimisha miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano

 wa Tanzania,huku yakielezwa mafanikio mbalimbali ndani ya Muungano huo ukiwemo mshikamano miongoni mwa Watanzania na ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Akizungumza na wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha,Katibu Tawala wa Mkoa huo,Ndg. Balandya Elikana amebainisha mshikamano wa Kitaifa tulionao umeondoa ubaguzi licha ya kuwepo na wingi wa makabila hapa nchini.

"Ndugu wananchi tuna kila sababu ya kuulinda na kuutetea Muungano wetu,mtu wa kutoka Bara anaweza kwenda Zanzibar na mtu wa kutoka visiwani humo ana uwezo wa kuja huku bila ya vikwazo vyovyote,hali hii ndiyo imelijenga Taifa imara la Tanzania.

Amesema waasisi wa Muungano huu Hayati Baba wa Taifa,Julius Nyerere na Abeid Aman Karume tuwaenzi kwa kuzidi kuimarisha Umoja wetu huku ukileta tija kwa kila upande.

"Miongoni mwa mafanikio ya Muungano wetu tunaona miradi mbalimbali ya kuwaletea maendeleo wananchi ikifanyika,hapa Mwanza tuna ujenzi wa Reli ya kisasa SGR,Daraja la JP Magufuli,Meli ya Mv Mwanza na upanuzi wa uwanja wa ndege,"Balandya.

Aidha ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia kwa kuzidi kuimarisha sekta za afya,  elimu na kilimo tukiadhimisha miaka 60 ya Muungano tukiona sekta hizo zikizidi kuwa na tija kwa kuleta mageuzi ya kimaendeleo kwa wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela ambapo sherehe hizo Kimkoa zimefanyika wilayani humo,Katibu Tawala wa Wilaya hiyo,Wakili Mariam Msengi amebainisha wameadhimisha sherehe hizo kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya usafi sehemu kadhaa, kupanda miti na kufanya mashindano ya burudani.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umefanyika Aprili 26,1964 chini ya waasisi Hayati Julius Nyerere na Abeid Karume.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano inasema Tumeshikamana,Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.