• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza yaja na Muarobaini wa Madini Chumvi

Posted on: May 11th, 2023

**Wiki ya madini Mwanza yaja na mwarobaini wa madini chumvi*

*


Maonesho ya wiki ya madini yaliyofanyika kitaifa mkoani Mwanza kuanzia Mei 3 hadi 9, 2023 yamekuwa na faraja kwa wachimbaji  na wafanyabiashara ya madini ya chumvi nchini baada ya kupitishwa kwa maazimio 14 ya kuendelea sekta ya madini ikiwemo madini hayo.

Akizungumza jijini hapa jana baada ya kumalizika kwa mkutano mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania(Femata) John Bina alisema maazimio hayo yamepitisha na wadau mbalimbali walioshiriki mkutano huo, wiki ya madini na kongamano la madini lililofanyika Mei9,2023.

“Tumepitisha maazimio 14 kati ya hayo maazimio 10 yameilenga serikali kupitia Wizara ya Madini na manne yanailenga Femata yote yatafanyiwa kazi ili kuwanufaisha wachimbaji,miongoni mwa maazimio ni wizara ya Madini

kuandaa mkutano mkuu wa  kitaifa utakaojadili changamoto na fursa zilizopo kwenye uchimbaji na biashara ya madini ya chumvi nchini.

“Madini haya yamesahaulika sana, licha ya umuhimu wake kwenye mwili wa binadamu lakini yamekuwa hayapewi kipaumbele wakati tunayo mengi hapa nchini hivyo tunaamini hatukukaa hapa Mwanza kwa kwa siku nane bure siku hizo zitazaa matunda,” alesem Bina na kuongeza

 “Wachimbaji wa madini hayo na wafanya biashara watakwenda kunufaika kwa sababu serikali ikitambua changamoto na fursa zilizopo kutoka kwa sisi wachimbaji itazifanyia kazi maana serikali yetu inatusikiliza siku zote sisi wachimbaji wadogo na lengo letu la la kuchangia pato la taifa kwa asilimia 20 ifikapo mwaka 2028 tutalifikia,”alisema Bina

Maazimio mengine yaliyopitishwa ni pamoja na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kuendelea kufanya utafiti wa madini kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo wa madini na taarifa za tafiti ziwafikie wadau kwa wakati, mchakato wa utoaji  leseni kwa wachimbaji wadogo uwe wa wazi na unaozingatia sheria, kanuni na taratibu ili kuendana na haki kwa wachimbaji wadogo wanaoomba leseni kupitia Tume ya Madini.

Pia Wizara ya Madini  kukamilisha zoezi la kupitia tozo zinazotozwa na halmashauri kwa wachimbaji wadogo ili isiwe kikwazo  katika uchimbaji mdogo wa madini .

Aidha Bina aliishukuru Serikali ya Mkoa wa Mwanza inayoongozwa na Mhe. Adam Malima  kwa  usalama waliopata muda wote wa siku tisa walipokuwa mkoani humo   .

Mgeni rasmi aliyefunga mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha  Wachimbaji Madini Wanawake Tanzania, (TAWOMA) Taifa Semeni Malale, alisema ili Femata iweze kutimiza malengo iliyojiwekea  ni vyema  wanachama wote wakashirikiana na kusameheana huku wakifanya shughuli zao kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.