• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza kukabiliana na 84% ya Magonjwa ya Kichocho na Minyoo..

Posted on: July 18th, 2017

Mkoa wa Mwanza umezindua kampeni ya umezeshwaji wa dawa za kukinga na kutibu ugonjwa wa kichocho na minyoo ya tumbo kwa watoto walio na umri kati ya miaka 05-14 huku wakiwa na malengo ya kuwapatia dawa hizo watoto zaidi ya laki saba katika shule zipatazo 955 za msingi ili kukabiliana na asilimia 84 ya watoto wanaodhaniwa kuwa na maambukizi hayo.


Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amesema zoezi hilo ni utekelezaji wa kampeni za kitaifa hususani ni katika magonjwa ambayo hapo awali yalikuwa hayapewi kipaumbele lakini sasa serikali imeamua kwa dhati kukabiliana nayo.

“Magonjwa haya kimsingi hudhorotesha sana afya za watoto na hii nikutokana na asili ya watoto kupenda kucheza katika maji au kupita katika maji pasipo kuwa waangalifu, alisema Mkuu huyo wa mkoa na kuongeza kwamba, kutokuwa na afya njema hupekea hata nguvu kazi ya uzalishaji kupungua, kutokana na kutokuwa na watu watakao shiriki shughuli za maendeleo.

Mkuu huyo wa mkoa amesema, kutochukua tahadhari za mapema, nguvu kazi nyingi huishia katika kujitibu jambo linalochukua rasilimali watu, muda na fedha kwaajili yakuangalia afya hapo badae, hivyo zoezi linalofanyika kwa sasa nikuliepusha taifa na madhara makubwa ya badae.

“Rasilimali fedha zinazo tumika wakati wa ugonjwa zingeweza kutumika na mgonjwa mwenyewe au familia kufanya shughuli za maendeleo” aliongeza Mongella.

Mwisho mkuu huyo, amemalizia kwakusema, kwa upande wa watoto hupunguza sana uwezo wao katika masomo lakini pia katika suala la michezo, hivyo kuyataja kama magonjwa yenye hasara kubwa katika jamii yetu.

Awali akitoa maelezo ya utangulizi Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Leonard Subi, amesema usugu wa magonjwa mengi ya utu uzima chimbuko lake ni kutokana na kutochukua tahadhari za mapema.

Subi amesema tafiti zinaonesha kuwa watu katika mwambao wa ziwa Viktoria wamekuwa waathirika wakubwa  wamagonjwa hayo, huku akizitaja Wilaya za Magu, Ilemela, Nyamagana Sengerema na Buchosa pamoja na Ukerewe katika mkoa huu kuwa waathirika wakubwa.

“Takribani ni watoto asilimia 84, wameambukizwa kichocho pamoja na minyoo huku kichocho kikitajwa kuwa juu zaidi ya minyoo” amesema Subi na kuongeza kuwa, Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wanapatiwa dawa za minyoo na zoezi la safari hii sio zoezi lakwanza.

Subi amesema, wagonjwa wengi zaidi ya asilimia 80 wanaofika hospitalini kwaajili ya maradhi ya saratani ya kibofu cha mkojo historia inaonesha waliwahi kuugua kichocho walipokuwa wadogo, “Mhe. Mkuu wa mkoa Kichocho pia kinaweza kuathiri mfumo mzima wa ubongo” hivyo tunaomba watoto tuwaangalie na wakati mwingine tuwe mstari wa mbela katika kuwakataza na michezo ya kwenye maji.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makaazi Mhe. Dkt. Angelina Mabulla katika salaam zake zilizo tolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, ameunga mkono zoezi hilo, huku akisema kuwa watoto ndio nguvu kazi ya taifa la kesho hivyo tunakila sababu yakuzingalia na kuzilinda afya zao wangali wadogo, “Taifa lisilo wekeza kwa watoto wake ni taifa mufilisi” alisema Mabulla.

Mkoa wa Mwanza, umefanya zoezi hilo, huku ukiwa umesambaza dawa hizo katika vituo vyote vya afya pamoja na shule zote 955 za msingi kwenye mkoa wa Mwanza huku wakiwa na lengo lakuwafikia watoto zaidi ya laki saba waliopo shuleni na wale ambao wapo majumbani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.