• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WAIPONGEZA BUCHOSA KWA UHIFADHI WA MAZINGIRA, WAPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI MOJA KWA MWAKA

Posted on: July 16th, 2023

MWENGE WA UHURU WAIPONGEZA BUCHOSA KWA UHIFADHI WA MAZINGIRA, WAPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI MOJA KWA MWAKA


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Buchosa kwa juhudi kubwa wanazofanya katika kutunza na kuhifadhi mazingira.

Ndugu Kaimu ametoa pongezi hizo mapema leo katika shule ya Sekondari Bukokwa wakati akishiriki zoezi la upandaji miti 500 iliyotolewa na wakala wa huduma za misitu nchini (TFS) kati ya 1000 iliyopandwa kwenye shule hiyo katika kutekeleza ujumbe wa Mwenge wa mwaka huu.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa amesema, viongozi na watendaji wameonesha kwa dhati nia ya kuhifadhi Mazingira kwani miti 1513700 imepandwa ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa 2022/23 katika maeneo mbalimbali kama kwenye miradi ya maji.

"Hongereni sana Buchosa, ninyi ni mabingwa wa uhifadhi wa mazingira." amesisitiza kiongozi huyo wa Mbio za wmenge wa uhuru zinazoenda sambamba na kaulimbiu isemayo

"Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Uchumi wa Taifa."

Akitoa taarifa ya mradi huo, kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Walter Njau amesema Halmashauri hiyo imejikita katika kutunza vyanzo vya maji, kurejesha uoto wa asili na Ikolojia ya viumbe hai na utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ya aina mbalimbali ikiwemo ya matunda, miti ya mbao na miti ya asili.

Katika wakati mwingine, wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini wilayani humo wameonesha nia ya kumtua mama ndoo kichwani wananchi zaidi ya 4118 kwa kuwaletea huduma ya maji safi kwa kuwajengea mradi wenye thamani ya zaidi ya milioni 190 ambao umewekewa jiwe la msingi (zaidi ya 85%) na Mwenge wa Uhuru ambao tayari umeshaanza kutoa maji.

Katika wakati mwingine, Halmashauri hiyo imedhihirisha shauku yao ya kutaka kuhifadhi vyanzo vya maji baada ya kuufikisha Mwenge kwenye mradi wa umwagiliaji unaolenga kuwanufaisha zaidi ya wakulima 700 kwa kupata chakula cha kutosha kabla ya kuzindua madarasa mawili Rwenchenga na kuweka mawe ya msingi kwenye bweni la wanafunzi Nyehunge.

Baada ya kushindwa kuzindua mradi wa jengo la huduma za dharula kwenye Hospitali ya wilaya kwa kukosa sifa za ubora na viwango stahiki kutokana na thamani ya fedha kiasi cha nilioni 300, Mwenge wa Uhuru umeiagiza Halmashauri ya Buchosa kujenga tabia ya kusimamia miradi vizuri ili iwe na tija kwa wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.