• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA KUKU WA MAYAI WA ZAIDI YA MILIONI 700 MISUNGWI

Posted on: July 18th, 2023

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA KUKU WA MAYAI WA ZAIDI YA MILIONI 700 MISUNGWI


Leo Julai 18, 2023 Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa ufugaji kuku wenye thamani ya zaidi ya Milioni 700 katika kijiji cha Idetemia Usagara Wilayani Misungwi ambazo kati ya fedha hizo asilimia 65 ni mkopo toka Benki ya Kilimo Tanzania (TADB).

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Abdalla Shaibu Kaim amempongeza mwekezaji (Angroberg Farm Ltd) kwa uwekezaji huo mkubwa na wa kisasa ambapo hadi sasa mradi huo una jumla ya kuku 20,000.

Ndugu Kaim amesema, kuamua kuwekeza fedha kubwa kiasi hicho ni dalili ya kuwa imara kimaono na ubunifu na hasa baada ya kukagua na kugundua kuwa mradi huo umezingatia usalama, afya na utunzaji na uhifadhi wa mazingira.

"Huu si ufugaji tu bali ni wa kisasa, hongereni sana kwa ubunifu na uwekezaji mkubwa ambao umezingatia utunzaji na uhifadhi wa mazingira na kwa hakika Mwenge wa Uhuru umeridhika na ubora wa mradi." amesisitiza Ndugu Kaim.

Katika wakati mwingine Mwenge wa Uhuru umezindua madarasa aita kwenye shule ya Sekondari Idetemia yenye thamani ya zaidi ya Milioni 123 na kiongozi wa nbio za Mwenge wa Uhuru 2023 akatoa rai kwa Mkuu wa Wilaya hiyo kuongeza usimamizi kwenye miradi hususani eneo la manunuzi ya vifaa.


Aidha, kutokana na dosari zilizobainika kwenye mradi huo Ndugu Kaim ametoa siku nne kwa wilaya hiyo kuhakikisha wanazirekebisha ili kuhakikisha kunakua na ubora ili wanafunzi wapate mazingira wezeshi kwa kujifunza na kujifunzia na kuongeza ufaulu kwenye shule hiyo.

"Mhe. Mkuu wa Wilaya endelea kusimamia miradi yetu ili ikamilike kwenye ubora hususani kwenye upande wa manunuzi ya vifaa hakikisha bei zinazingatia nyaraka za vifaa vya ujenzi (BOQ) ili fedha zitumike vizuri," amesema Ndugu Kaim, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023.

Baada ya ukaguzi wa kikundi cha wasafirishaji abiria (Bodaboda) Ngudama-Bulemeji Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye jengo la mionzi kwenye kituo cha afya Misasi na kuagiza usimamizi mzuri ili hatimaye iweze kukamilika kwa wakati lakini kwa ubora madhubuti.

Mwenge wa Uhuru umeipongeza Halmashauri ya Misungwi kwa kubuni mradi wa vibanda vya biashara kwenye stendi ya mabasi vinavyojengwa kwa zaidi ya Milioni 75 ambapo mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi na kubainisha kuwa utasaidia kuongeza mapato ya ndani na kujihakikishia kujitegemea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.