• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwenge wa Uhuru wataka taratibu za Miradi zifuatwe Wilayani Misungwi

Posted on: July 13th, 2022

Katika kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na viwango elekezi viongozi wenye dhamana ya usimamizi wa miradi wametakiwa kufuata maelekezo ya miradi mbalimbali yanayotolewa  kuhusu miradi hiyo ili kuepuka maswali mengi yanayoleta wasiwasi wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo.

Hayo yamesemwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu  Sahili Geraruma mapema hii leo mara baada ya kukagua miradi inayopitiwa na Mbio za Mwenge Wilaya ya Misungwi.

Akiwa katika Shule ya Sekondari Manawa ambapo amekuta Ujenzi ukiendelea katika mradi huo uliogharimu shilingi milioni 471.8, ndugu Geraruma amewataka wenye dhamana ya usimamizi wa miradi kufuata taratibu zilizowekwa.

"Viongozi na wasimamizi wote wa miradi, hakikisheni  mnafuata taratibu zote zinazotakiwa kuhusiana na miradi ikiwemo kuomba kuongezewa muda pale,mnaposhindwa kukamilisha kwa wakati na siyo kukaa kimya,''amesema Geraruma.

Aidha,ameshauri na kuwataka Viongozi wa Halmaahauri hiyo kusimamia vizuri Miradi ambapo amepongeza baadhi ya Miradi hiyo ikiwa ni pamoja na Miradi ya sekta ya Afya, Elimu, Maji, Uwezeshaji Wananchi kiuchumi na Mradi wa Ujenzi wa Barabara.

Pamoja na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa kuhusiana na Miradi hiyo, Miradi iliyowekewa jiwe la Msingi, na kuzinduliwa ni pamoja na Ujenzi wa Shule ya Sekondari Manawa, Ujenzi wa Barabara ya Lami, Ujenzi wa Kituo cha Afya Usagara, Mradi wa Ujenzi wa Chuo cha Afya MacWish, Mradi wa usambazaji Maji wa Fella, Ujenzi wa Madarasa 8 katika Shule ya Sekondari Sanjo, na Mradi wa  usafi wa mazingira na usafirishaji mizigo.

Hata hivyo,Miradi hiyo imetokana na mchango wa jamii  shilingi Milioni 11.3 na Halmashauri imetoa shilingi Milioni 16.7 ambapo Serikali Kuu imechangia shilingi Bilioni 1.6 na wahisani wamechangia shilingi Bilioni 1.5 na Miradi yote inaendelea kutekelezwa na baadhi imekamilika.

Akihitimisha ukaguzi wa miradi  Geraruma amewataka wenye dhamana ya miradi hiyo kuhakikisha wanafanya marekebisho katika mapungufu yote yaliyobainika wakati wa ukaguzi ikiwa ni pamoja na kufuata na kuzingatia kanuni taratibu za Ujenzi ili kukamilisha Ujenzi huo na kupata Miradi inayokidhi na yenye Viwango.

Mwenge wa Uhuru utaendelea na mbio zake katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu kesho tarehe 14/7/2022 baada ya kukamilisha mbio hizo Wilaya ya Misungwi  ukitokea Wilayani Kwimba ambapo umekimbizwa km 75.3 na kupitia miradi 7 yenye thamani ya shilingi bilioni 3.12.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.