• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

NEMC yashauriwa kuziongezea meno baadhi ya Sheria zake za kulinda Mazingira.

Posted on: May 5th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amelishauri Baraza la Taifa la Hifadhi ya usimamizi wa Mazingira Tanzania,NEMC kupitia upya baadhi ya Sheria zake za utunzaji wa Mazingira hasa za Kelele sumbufu ambazo zimekuwa kero kwa wananchi siku hadi siku.

Akizungumza kwenye kikao kazi cha Baraza hilo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa uliokuwa unajadili uwepo wa matumizi ya mifuko ya Plastiki na Kelele sumbufu,Mhe.Malima amesema utoaji wa vibali kwa kumbi za starehe na nyumba za ibada usiozingatia Sheria na taratibu umechangia kusababisha kero kwa wananchi na ushahidi ni ofisi yake inayopokea malalamiko hayo kila uchao.

"Kelele sumbufu kwa kweli zinawatesa sana wananchi,kaeni pitieni vizuri Sheria zenu na ikibidi mkaziongezee adhabu zaidi,baadhi ya nyumba za ibada zinakiuka kabisa taratibu kwa kupaza sauti usiku kucha bila kujali athari zake kwa walio jirani,hii kwa kweli haikubaliki",amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kuhusu mifuko ya Plastiki Mhe.Malima ameishauri NEMC kuona namna ya kuwajali wafanyabiashara wadogo  ambao wamekuwa wakitumia baadhi ya vifungashio vya plastiki kwenye bidhaa wanazouza kwa kuangalia mpango mbadala na kuboresha baadhi ya vibebeo ambavyo havitakuwa na madhara kwenye mazingira.

"Bwana Kayombo hii jaribuni mkae na kulitazama vizuri hasa utoaji wa elimu kwa wananchi,nakubali kuna baadhi ya vibebeo havistahili kama vifungashio kwenye pilipili au vitunguu lakini bidhaa kama Njegere ili imvutie mnunuzi ikiwemo kwenye kibebeo cha kuonekana ana uhakika wa biashara yake kutoka  maana wafanyabiashara hawa wengi mitaji yao ni midogo hawana ubavu wa kuweka bidhaa zao kwenye vyombo maalum ",Mhe.Malima.

Aidha Mhe.Malima ameliahidi Baraza hilo la Mazingira kushirikiana nalo akiwashirikisha viongozi wa Kamati ya Amani Mkoani Mwanza kuzifanyia ukaguzi na kuchukua hatua baadhi ya nyumba za ibada zisizo na sifa na kugeuka kero kwa wananchi.

"Tupo hapa Mwanza kwa muda wa siku saba kufanya ukaguzi kwa wanaokiuka matumizi ya mifuko ya Plastiki na Kelele sumbufu,tunashirikiana na kamati ya ulinzi na usalama wale wote watakaobanika mkondo wa Sheria utawapitia ikiwemo kufunga  kumbi za starehe na nyumba za ibada na kuwachukulia hatua kali ikiwemo kifungo,"Hamad Taimour,Meneja uzingatiaji Sheria NEMC

"Nimefurahishwa na Mhe.Malima kutuletea hapa ukumbini uthibitisho wa matumizi yenye usahihi na usio sahihi wa hivi vibebeo vya plastiki,sisi kama NEMC hii changamoto tumeiona na tutaifanyia kazi lengo ni kuhakikisha mazingira yetu yanabaki salama kwa faida yetu na vizazi vijavyo, bidhaa zote ambazo haziozi ardhini kuhakikisha hazitumiki",Jerome Kayombo,Meneja Kanda NEMC

Baraza la Taifa la Hifadhi ya usimamizi wa Mazingira Tanzania NEMC, lilipitisha sheria ya katazo la matumizi ya mifuko yote ya Plastiki mwaka 2019 baada ya kubainika inachangia kwa kiasi kikubwa uchafuzi na uharibifu wa Mazingira.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.