• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Nyamagana yatakiwa kutoa elimu kwa wanufaika wa TASAF

Posted on: February 21st, 2023


Uongozi wa Halmashauri ya Nyamagana Mkoani Mwanza umetakiwa kutoa elimu kwa wanufaika 2880 wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF baada ya Serikali kutoa fedha Shs milioni 168.1 za kuinua uchumi kwa walengwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Jenista Mhagama akizungumza na wananchi Wilayani humo mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, Ofisi moja, Mabweni pamoja na bwalo la chakula kwenya shule ya Sekondari Nyamagana miradi inayofadhiliwa na TASAF amesema lengo la Serikali ni kuona uchumi wa mtu mmoja mmoja unapiga hatua ndiyo maana imekuwa ikitoa fedha nyingi kupitia miradi hiyo.

"Nataka kuona wanufaika  wote 2880 wanaotarajiwa kupata fedha hizo wanaelimishwa vyema,h hizi fedha siyo za kunywea pombe bali zilete mageuzi ya kiuchumi kwa kufanya miradi itakayoongeza kipato ndani ya familia." Mhe. Mhagama.

Amebainisha kuwa mara baada ya kukagua Shule ya Sekondari ya Nyamagana ameziona kasoro ndogo ikiwemo udogo wa bwalo la kulia chakula na kuwataka walikamilishe na Serikali italeta fedha nyingine kati ya Juni au Julai mwaka huu ili lijengwe lingine kubwa zaidi.

"Mhe. Waziri sisi Nyamagana tunaishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa namna inavyoonesha kutujali kwa vitendo,tupo mbioni kukamilisha ujenzi wa madarasa ya maghorofa kwa shule 13 na kila darasa litakuwa na wanafunzi 42 na tutakuwa wilaya yenye mfano hapa nchini kwa kuwa na shule bora".Amesema Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi.

TASAF imegharamia Shs Milioni 426,163,729.48 kujenga miundo mbinu shule ya Sekondari ya Nyamagana vikiwemo vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita na hadi sasa zimetumika Shs milioni 258,904,204.29 na utekelezaji umefika asilimia 60.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.