• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

OR TAMISEMI Yatoa Mafunzo ya Ugatuaji wa Madaraka

Posted on: April 18th, 2019

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imesema inataka zana ya Ugatuaji iwe na mamlaka ya kutekeleza shughuli zake kisera na kisheria.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa huduma za Sheria kutoka Tamisemi Edwin Mgendera kwenye mawasilisho ya wataalamu washauri katika kuboresha rasimu ya awali ya sera ya Taifa ya Ugatuaji wa madaraka kwa viongozi na wadau wa Mikoa mitano ya Kanda ya Ziwa (Simiyu, Mwanza, Kagera, Geita na Mara).

Mgendera alisema, ugatuaji sio jambo geni, awali ulikuwepo japo hapakuwa na sera wala sheria, hivyo walikuwa wanatekeleza shughuli hizo za ugatuaji wakitegemea andiko la ugatuaji wa madaraka la mwaka 1998.

“Tunataka kutengeneza sera ya ugatuaji wa madaraka kutoka serikali kuu kuja kwenye vyombo mbalimbali, inaweza kuwa wakala wa serikali, mamlaka ya serikali za Mitaa au watu Binafsi tofauti na pale awali unamuingizaje mtu binafsi kwenye suala la ugatuaji, tunataka sasa iwe kisera alafu sheria ifafanue,”alisema Mgendera.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Dkt. Philis Nyimbi aliwataka viongozi ambao ni wawakilishi wa wananchi na wadau kutoka Asasi za Kiraia kutoa mapendekezo na maoni yatakayo boresha rasimu hiyo kwa maendeleo ya Taifa.

 “Kila mmoja wetu anao mchango mkubwa wa kuleta wazo au kupendekeza ili mwisho wa siku Taifa letu lipate rasimu ambayo hata wananchi wakiisikia wataona vitu vimenyooka,ambavyo vimelenga asili yetu”alisema Dkt. Nyimbi.

Naye Juma Iddi kutoka idara ya Uratibu wa sekta Tamisemi alisema, ugatuaji madaraka umeleta mafanikio kidemokrasia na kwenye maeneo ya utoaji wa huduma ambayo Wizara za kisekta ziliwezesha  mamlaka za msingi.

“Kwa sera ambayo tulikuwa nayo ilikuwa na mafanikio, wananchi wanashiriki vizuri katika shuguli za kidemokrasia za kuchagua na kuchaguliwa katika uongozi, wanajiongoza lakini pia katika utoaji wa huduma, Serikali inaweza kupeleka fedha moja kwa moja bila kupitia mahali pengine”alisema Iddi.

Aliongeza kuwz wanataka mafanikio waliyoyapata kwenye maeneo walioyagatua kama kwenye eneo la elimu wapate pia kwenye kilimo, mifugo na uvuvi na njia nzuri ni kuunganisha nguvu ya wadau wote kwakuwa na sera ya pamoja ili kila mmoja ajue wajibu wake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.