• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto yazinduliwa Mwanza

Posted on: September 23rd, 2023

Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto yazinduliwa Mwanza


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana ametoa wito kwa wazazi na wadau wa watoto kushirikiana kuhakikisha kunakua na upatikanaji wa lishe bora kwa watoto ili kuwajengea afya na Siha njema ya malezi na makuzi mazuri ili kujenga Taifa imara.

Ametoa wito huo leo septemba 22, 2023 wakati akizindua Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT- MMMAM) 2021/22-2025/26 ngazi ya Mkoa katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa.

"Ndugu wadau, naomba tutambue kuwa Maendeleo ya mtoto yanategemea msingi imara unaowekwa kwa malezi bora ya tangia umri wa utoto hivyo ni muhimu kuzingatia malezi bora ya watoto wetu kila siku ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa lishe bora wakati wote" Amesisitiza Ndugu Elikana.

Aidha, amesisitiza juu ya ulinzi wa watoto kuanzia kwenye ngazi za kaya kuhakikisha malezi ya watoto yanawaweka salama na kila aina ya Ukatili ili watoto wawe na makuzi bora yatakayowajengea ujasiri wa kutegemewa kuinua uchumi kwa kujihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Joel Mwakapala amesema kuwa programu hiyo inayokadiriwa kugharimu zaidi ya Bilioni 914.9 kutoka kwa wadau mbalimbali ilizinduliwa rasmi kitaifa na Waziri Doroth Gwajima kwa niaba ya Dkt. Samia Rais wa Tanzania kuhakikisha watoto wote tanzania kuanzia miaka 0 hadi 8 wanafikia utimilifu wao.

Aidha, amebanisha kuwa kutokana na umuhimu mkubwa wa eneo hilo programu hiyo jumuishi inashirikisha Wizara za kisekta kama Ofisi ya Waziri Mkuu eneo la Sera, Ajira, Makundi maalumu na Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu, Wizara ya Fedha pamoja na Wizara ya Mipango na uwekezaji ili kuhakikisha malengo yanatimia.

Amefafanua kuwa utafiti umefanyika kwenye maeneo ya Afya bora, Malezi yenye muitikio, ujifunzaji wa awali, ulinzi na usalama, Lishe bora na makuzi na malezi ya mtoto yenye Muitikio na ndipo imabainika katika kipindi cha umri huo ndipo ukuaji wa mtoto yanafanyika na inahitajika ukamilifu wa huduma zote ili kumhakikisha mtoto kuwa salama.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwasilisha ombi kwa wadau wa watoto kuhakikisha wanahusisha afua za usimamizi na uboreshaji wa watoto kwenye shughuli zao ili kuhakikisha kundi hilo linalindwa na kiendelezwa vizuri kwa ajili ya maendeleo ya Taifa la sasa na baadae.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.