• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUMALIZA KERO YA MAJI MWANZA : RC MAKALLA

Posted on: December 18th, 2023

RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUMALIZA KERO YA MAJI MWANZA : RC MAKALLA


*Ampongeza Rais Samia kutoa fedha Bilioni 70 upanuzi chanzo cha maji Butimba*


*Ametoa fedha kupanua Chanzo cha maji Capripoint*


*Aelekeza ujenzi wa Matanki 5 makubwa uanze*


*Atinga Site kukagua ukarabati wa bomba lililoharibiwa na mvua Kishiri*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa chanzo cha maji Butimba uliokamilika Oktoba 30, 2023 ukijengwa kwa zaidi ya Bilioni 70 na kuzalisha Lita Milioni 48 kwa siku na akatumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha hizo.


Akizungumza leo kwenye chanzo cha mradi huo kilichopo kwenye kata ya Butimba Makalla amesema Mhe. Rais ameamua kwa dhati kumtua Mama ndoo kichwani kwa kumuondolea adha ya upatikanaji maji mkoani humo jambo ambalo awali lilikua ni kama ndoto kulifikia.

"Leo ni mara ya nne nimefika hapa ikiwa ni katika kusukuma ili mradi ukamilike, nawapongeza wote kuanzia Mkandarasi na viongozi kwa kutekeleza mradi huu ambao ni wa kisasa kabisa kwa jinsi mitambo niliyoiona ikifanya kazi, nachotaka sasa tuongeze nguvu kwenye ujenzi wa matanki na usambazaji," amesema Makalla.

Katika kuhitimisha ziara yake kwenye miradi ya maji Mwanza, Mkuu wa Mkoa amefika kweye mtaa wa Kishiri Bushitu kukagua ukarabati wa bomba lililoharibiwa na mvua na ameahidi kurekebisha hali hiyo mapema iwezekanavyo na akabainisha kuwa wananchi wa eneo hilo wanatarajiwa kujengewa barabara kwa kiwango cha lami KM 22 kutoka Buhongwa siku za usoni

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) Nelly Msuya amebainisha kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha si tu wananchi waliotajwa kwenye usanifu bali hata wengine nje ya mradi kwa kushirikiana na usambazaji wa maji yatokayo kwenye chanzo cha Capripoint.

Awali Mhandisi Selestine Mahubi ambaye ni Msimamizi wa mradi huo alifafanua kuwa wananchi wa mitaa ya Igoma, Kishiri, Ndose, Nyamaliwa, Nyamhongolo, Kisesa, Kanyama, Malimbe na Luchelele wananufaika na kwa upanuzi wa awamu ya pili watanufaika Usagara, Fela, Bukumbi, Nyashishi na Misungwi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.