• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA AONGOZA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWANZA

Posted on: October 14th, 2024

RAIS SAMIA AONGOZA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWANZA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo  Oktoba 14, 2024 amewaongoza watanzania katika kilele cha kishindo cha mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 sherehe zilizofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba uliopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela.

Akiongea na wananchi Mhe. Rais amewataka watendaji katka Halmashauri zote nchini kutekeleza miradi kizalendo kwa kuzingatia sheria na kanuni na katika kuwainua vijana amebainisha kuwa umefika wakati sasa kwa halmashauri nchini kununua vifaa kutoka kwenye kundi hilo ili kuwainua kiuchumi kwa kuongeza kipato.

Akitoa risala kwa Mhe. Rais, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 Godfrey Mnzava amesema wananchi kote nchini wametoa salamu za pongezi kwa Serikali kwa kuboresha huduma za kijamii kama maji, elimu, afya pamoja na miundombinu ya barabara na wameomba kuboreshewa sehemu chache zenye changamoto.

Aidha, amebainisha kuwepo kwa kasoro kwenye miradi 16 kati ya zaidi ya miradi 1500 ambayo Mwenge wa Uhuru umetembelea mwaka huu na kwamba TAKUKURU wamegizwa kufuatilia nyaraka za miradi hiyo ili waliohusika kufanya ubadhirifu wachukuliwe hatua ikiwemo kutofuata taratibu za manunuzi ya umma.

"Pamoja na ukaguzi wa miradi, kupitia mikesha lita 5,832 za damu zimekusanywa kutokana na uchangiaji wa wananchi ambazo zitasaidia wahitaji kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini." Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Mwenge wa Uhuru mkoani humo umefika kwenye miradi 53 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 99 na akabainisha kuwa asilimia 30 ya wananchi wamejiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa mnamo novemba 27, 2024.

Hali kadhalika Rais Samia amemkabidhi Mwenge wa Uhuru na Bendera Mkuu wa majeshi ya ulinzi JWTZ ,Jenerali Jacob Nkunda ili ukapandishwe kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro kama ishara ya kutimiza miaka 60 tangu kupandishwa hapo juu


Mwenge wa Uhuru umekagua nchi nzima miradi yenye thamani ya shs trilioni 11

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu zilianza mkoani Kilimanjaro kwa kuzindua mradi wa sekta ya Elimu kwenye manispaa ya Moshi tarehe 02 Aprili, 2024 na kuhitimishwa jana katika halmashauri ya manispaa ya Ilemela-Mwanza kwa kuzindua ujenzi wa barabara ya lami nzito (Asphalt Concrete) ya Kiyungi (0.49).

Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu  uliokagua miradi ya jumla ya shs trilioni 11 nchi nzima, "Tunza mazingira na shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa ujenzi wa Taifa endelevu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.