• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AFANYA ZIARA YA GHAFLA KITUO CHA AFYA IGOMA, AWAPONGEZA WATUMISHI

Posted on: September 9th, 2024

RAS BALANDYA AFANYA ZIARA YA GHAFLA KITUO CHA AFYA IGOMA, AWAPONGEZA WATUMISHI

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana usiku wa Jumapili Septemba 8,2024 amefanya ziara ya ghafla kwenye kituo cha afya Igoma na kuridhishwa na utendaji kazi wa watumishi waliokuwa zamu muda huo na kuwataka kuongeza bidii ya kuwatumikia wateja wao.

Akiambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jesca Lebba,Balandya alianzia sehemu ya mapokezi ya wagonjwa kutoka nje OPD na kufanya mazungumzo nao namna walivyopokelewa na utaratibu mzima waliopatiwa kituoni hapo huku kila mteja akipongeza huduma sahihi walizopata.

Mtendaji huyo wa Mkoa alipita sehemu za wodini na wodi ya wazazi na huko pia alizungumza nao kabla ya kukagua sehemu ya kutolea dawa na kila eneo alishuhudia madaktari wa zamu na wasaidizi wao wakiendelea na kazi.

"Nawaombeni msiingie shaka kwa ujio huu na hasa kwa muda kama huu wa usiku, hii ni sehemu ya wajibu wetu kama viongozi na niwapongeze kwa kazi nzuri ya kuwahudumia wateja wenu,"amesema Balandya wakati akizungumza na watumishi wa kituo hicho na baadhi kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu.

Balandya amebainisha mara ya mwisho alipofanya ziara kwenye kituo hicho alipewa taarifa za changamoto mbalimbali za kiutendaji ukiwemo upungufu wa watumishi na uboreshaji wa mazingira ya kazi ambayvyo vyote vimefanyiwa kazi na mengineyo yapo mbioni kuboreshwa kulingana na bajeti ya Serikali.

Daktari wa zamu wodi ya wazazi,Mwita Chacha amesema wateja wake aliowapokea amawafanyia uchunguzi na wapo katika hali nzuri, na baadhi amewapa maelekezo ya kufanya mazoezi ili kurahisisha mzunguko wakati wa kujifungua

"Nampongeza Mganga Mkuu wa mkoa kwa kazi nzuri tangu umefika kituo chako kipya cha kazi hapa Mwanza sasa ni miezi miwili lakini umezunguka Halmashauri zote ili kujionea utendaji kazi na kutoa maelekezo," Balandya.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jesca Lebba amesema yeye na timu ya wataalamu kutoka Ofisini kwake wameweka utaratibu wa kufanya ukaguzi na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa watumishi wa vituo na hospitali zote za Serikali ili kuhakikisha kunakuwa na muendelezo wa utolewaje mzuri wa huduma bora kwa wateja wao.

"Ndugu Katibu Tawala, Mkoa wetu umekuwa hauna rekodi nzuri katika uzazi wa mama mjamzito,tumejipanga vizuri kuhakikisha vifo vinatoweka kwa kiwango kikubwa kama ulivyojionea madaktari wa zamu wapo muda wote wodi ya wazazi na wote wamefanyiwa uchunguzi na wenye changamoto zimefanyiwa kazi ili wajifungue salama,"Dkt.Lebba

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.