• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya ahimiza umakini wa kuwapata Watumishi wenye Weledi

Posted on: April 24th, 2023


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana  amewataka madiwani na wawakilishi kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania  kuwa huru kutoa maoni yao kuhusiana na uboreshaji wa  kanuni za ajira.

 Hayo yamesemwa leo Aprili 24 2023 kwa niaba yake na Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza Utawala na Rasilimali Watu Bw. Daniel Machunda wakati akifungua semina ya mchakato wa ajira katika utumishi wa umma na ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya kuboresha kanuni za uendeshaji wa shughuli za sekretarieti,amewataka washiriki husika kuzingatia kile watakachojifunza ili wakachangie ufanisi wa kazi kwa kupata Watumishi wenye weledi.

Sekretari ya Ajira katika Utumishi wa Umma imeandaa semina hiyo ili kuhakikisha sheria, kanuni, taratibu na miongozo yote ya ajira inazingatiwa ikiwa hichi ndicho chombo kilichopewa mamlaka kisheria kuwezesha upatikanaji wa watumishi katika utumishi wa umma.

"Sekretarieti ya ajira imeona ni jambo zuri  kuwashirikisha na nyinyi wadau ili muwe huru kutoa maoni yenu ambayo yatapelekea kupata kanuni mpya zitakazo ongeza tija katika mchakato wa ajira". Amesema Bw. Machunda

Pia Bw. Machunda amewataka washiriki wa semina hiyo kuzingatia mafunzo yatakayotolewa na wawezeshaji ili iwe rahisi kwao kushiriki kikamilifu katika utoaji wa maoni  ambayo yataboresha kanuni.

Aidha naye Naibu Katibu wa Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma Mhandisi. Samweli Tanguye amesema wameandaa semina hiyo kwa ajili ya kujielezea kwa wadau jinsi wanavyoendesha amichakato ya ajira na kanuni wanazozitumia.

" Tupo hapa Mwanza kwa ajili ya kutoa elimu na kujielezea kwa wadau wetu juu michakato ya ajira inavyoendeshwa na kuwaonesha michakato  ya ajira na kanuni tunazozitumia ili na wao waweze kupata nafasi ya kutoa maoni yao". Amesema Mhandisi. Tanguye

Naye Diwani wa kata ya Bujora halmashauri ya wilaya ya Magu Mhe. Bunyanyakei John amesema  Sekretarieti ya Ajira ikiyafanyia kazi maoni ya washiriki  yataleta matokeo makubwa sana katika ajira.

"Kama sekretarieti ya ajira ikisimamia kweli maoni ya washiriki basi maoni hayo ambayo tutayatoa yataleta matokeo makubwa katika ajira". Amesema Mhe. John

Semina hiyo ya siku mbili inayofanyika ukumbi wa Maji House Jijini Mwanza, imewahusisha Madiwani, Wakuu wa Idara ya Rasilimali Watu kutoka Taasisi za Serikali na wawakilishi kutoka Ofisi za Wakuu wa Mikoa ya Mwanza, Tabora, Geita, Shinyanga, Simiyu, Mara na kigoma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.