• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya aishukuru Serikali kwa kuboresha huduma za Meli kwenye Maziwa Makuu

Posted on: November 14th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg Balandya Elikana ameahidi kutoa ushirikiano kwa bodi mpya ya Kampuni ya Huduma za Meli MSCL iliyozinduliwa rasmi leo Mkoani Mwanza ili iweze kutimiza malengo yake kikamilifu.

Akizungumza na wajumbe wa bodi hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi,Balandya amesema kutokana na Mkoa wa Mwanza kuwa kitovu cha biashara eneo la Afrika Mashariki na kati,huduma za usafiri wa majini ni kitega uchumi muhimu.

"Nichukue nafasi hii kuwahakikishieni bodi hii sisi kama Mkoa tuna kila sababu ya kuwapa ushirikiano hasa kwa kutambua Serikali ya ya awamu ya Sita ilivyoipa Mkoa huu miradi mingi ya Kimkakati yenye lengo la kusukuma mbele Maendeleo ya Wananchi"amesema Mtendaji huyo Mkuu wa Mkoa.

Amebainisha eneo la Maziwa yote matatu ya Victoria,Nyasa na Tanganyika nchi jirani za Malawi,Congo DRC na Burundi zinategemea sana mizigo yao kupitia kwenye Bandari zetu hivyo wajumbe wa bodi hiyo watambue jukumu walilonalo la kuifanya Kampuni hiyo kuwa bora kwa huduma na nguzo imara ya Uchumi wa Taifa letu.

Akizindua rasmi Bodi hiyo Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Uchukuzi Mhe.Atupele Mwakibete ametoa maagizo kadhaa kwa bodi hiyo ikiwemo usimamizi wa ujenzi wa Meli zilizopo Maziwa yote matatu,kusimamia ukarabati wa MV Lyemba na Mv Sangara pamoja na ubunifu wa Masoko.

"Serikali itanunua Meli mbili mpya za abiria itakayochukua watu 600 na tani 400 na ya mizigo itakayobeba tani 3000 zitakazotoa huduma Ziwa Tanganyika" amesisitiza Mhe.Mwakibete


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo Meja Generali mstaafu John Mbung'o amesema ana imani na wajumbe wake wenye taaluma zinazoendana na shughuli za Kampuni hiyo hivyo huduma za MSCL zitazidi kusonga mbele.

Bodi hiyo ya Kampuni ya Huduma za Meli itakaa madarakani kwa muda wa miaka miatu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.