• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AONGOZA KIKAO CHA WATUMISHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KUBORESHA KAZI.

Posted on: December 28th, 2023

RAS BALANDYA AONGOZA KIKAO CHA WATUMISHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KUBORESHA KAZI


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya  Elikana leo Disemba 28, 2023 ameongoza kikao cha watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo ambapo pamoja na mambo mengine amewapongeza kwa kazi na amewataka kuendelea kushirikiana katika kufanikisha shughuli za kila siku za kuhudumia wananchi.

Amesema katika kufanikisha hayo kila mmoja anapaswa kuhakikisha anajitoa kwa moyo wa upendo kuhudumia wananchi kwenye eneo lake na kuhakikisha aonapo changamoto anaifikisha sehemu husika kwa ajili ya kuzitatua na kuhakikisha kunakua na ufanisi kwa kufanyia maboresho kwenye eneo husika.

Balandya ameongeza kuwa katika kuhakikisha kuna usalama wa taarifa na uwasilishaji wa haraka na ufanisi wa mafaili ni lazima kutumia mfumo wa Mawasiliano wa Ofisi ambao unafikisha taarifa kwa mhusika na kwamba ofisi yake ipo kwenye mpango mahsusi wa kuboresha suala la vitendea kazi kama ununuzi wa magari ya Idara kadiri bajeti itakavyoruhusu.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi (TUGHE) tawi la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ndugu, Mangabe Mnilago amewataka watumishi kuendelea kujibidiisha kwenye kazi na Ofisi kuhakikisha wanatatua changamoto za Kimfumo ili kuhakikisha fedha zinapatikana kwa wakati na kufanikisha kusonga mbele kwa kazi.

Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Utawala na Rasilimali watu Ndugu, Daniel Machunda amewashukuru watumishi kwa kujituma na amebainisha kuwa Ofisi yake haina masuala mazito ya kinidhamu na ametumia wasaa huo kuwataka watumishi  kuwahi kazini ili kuhakikisha wanatimiza malengo ya siku katika kuboresha kazi.

Katika nyakati tofauti, watumishi wamewasilisha ombi la kununuliwa Basi ili kurahisisha uendeshaji wa shughuli zinazohitaji watumishi kwenda kwenye kazi kwa makundi kwani kwa sasa Mkoa umekua ukiazima usafiri kwenye taasisi zingine mathalani Sherehe za Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.