• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya atembelea maeneo hatarishi na Kipindupindu na kutoa maagizo

Posted on: February 14th, 2024

RAS Balandya atembelea maeneo hatarishi na Kipindupindu na kutoa maagizo


*Awaagiza Wavuvi wa Mwalo wa Mihama kuimarisha miundombinu ya Maji taka*


*Awataka Maafisa afya kuwachukulia hatua kali wasiokuwa na vyoo bora*


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Februari 14, 2024 amefanya ziara fupi ya kutembelea maeneo yaliyokumbwa na ugonjwa wa Kipindupindu Mihama kata ya Kitangiri na Kabuhoro-Kirumba na kuwataka maafisa afya kuwachukulia hatua za kinidhamu wale watakaobainika kutozingatia kanuni za usafi kwenye maeneo yao.

Mtendaji huyo wa Mkoa aliyeambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa Thomas Rutachunzibwa pamoja na Maafisa wa afya kutoka Halmashauri ya Ilemela amebaini kasoro kadhaa ikiwemo ukosefu wa choo bora na kutokuwepo kwa vifaa vya kunawa mikono licha ya eneo hilo kuwa na muingiliano wa watu wengi.

"Ndugu zangu nimefika hapa na kujionea hali isiyoridhisha, nawaagiza viongozi wote kwenye eneo hili rekebisheni haraka kasoro zote mkianzia miundombinu ya maji taka na vifaa vya kunawa mikono," amesisitiza Balandya wakati akizungumza na wakazi wa eneo hilo wengi wao wakiwa ni wavuvi.

Amewataka Maafisa afya kuwa wakali na kuchukua hatua bila kusita kwa wanaokwenda kinyume na miongozo iliyotolewa na kuzidi kutoa elimu kwa wananchi.

"Nimetembelea kaya kadhaa maeneo haya ya Mihama nimeona wasivyo zingatia usafi na nyumba nyingi hazina vyoo bora na nyingine hazina kabisa hii ni hatari na kukwamisha zoezi la kutokomeza ugongwa wa Kipindupindu," Katibu Tawala mkoa

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Thomas Rutachunzibwa amesema Ofisi yake imejipanga kuudhibiti ugonjwa huo na kuwataka watumishi wengine  kuongeza bidii katika maeneo yao ili kudhibiti maambukizi.

"Ndugu Katibu Tawala hii ni vita na jiografia ya Jiji letu wakazi wengi wapo maeneo karibu na mialo na milimani hivyo siyo sawa kuiwachia Idara ya afya pekee kupambana na hili, Maafisa uvuvi, MWAUWASA,TARURA na wengineo ni lazima kila mmoja awajibike ipasavyo katika eneo lake naamini tutafanikiwa," Dkt. Rutachunzibwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.