• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya awakumbusha Mafundi Sanifu kufanya kazi kwa uadilifu

Posted on: May 4th, 2023



Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amewataka mafundi sanifu kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na maarifa lakini pia wawe waadilifu ili waweze kutekeleza miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali kwa kiwango kilichokusudiwa.

Akizungumza kwenye mkutano mkuu wa tano wa mwaka wa mafundi sanifu uliowakutanisha washiriki zaidi ya 500 kutoka mikoa mbalimbali nchini unaofanyika jijini hapa kuanzia leo Mei 4 hadi 5,2023,  Elikana amesema miradi yote inayotekelezwa na serikali  kuna mchango mkubwa wa mafundi sanifu ambao wanaiwezesha kuendelea hivyo ni vyema wakawa waadilifu katika kutimiza majukumu yao.

“Naipongeza sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  kwa kazi kubwa inayofanya ya kuwaletea wananchi maendeleo,  katika mkoa  wetu wa Mwanza tumekuwa tukipokea mabilioni ya shilingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ya maendeleo.

“Tuna miradi ya kimkakati ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa daraja la JPM Kigongo- Busisi, reli ya kisasa, ujenzi wa meli mpya kubwa ya aina yake katika ukanda wa maziwa makuu MV MWANZA HAPA KAZI TU stendi ya mabasi ya abiria Nyegezi na mingine mingi inayotekelezwa na Tanroads na Tarura na hivi juzi tumesaini mkataba kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kilomita 54 kutoka Sengerema hadi Buchosa yote hii tunawategemea nyie mafundi sanifu,” amesema Elikana na kuongeza

“Ni matumaini yetu  miradi hiyo itakapokamilika itachochea sana ukuaji wa uchumi wa mkoa wetu, kanda ya ziwa na nchi kwa ujumla, tunaishukuru sana serikali lakini pia tunawategemea nyie mafundi sanifu mfanye kazi kwa bidii na muwe waadilifu ili tuweze kuitekeleza miradi hiyo na ionyeshe thamani halisi ya fedha,”ameeleza Elikana.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Mwanza aliwasihi washiriki wote wa mkutano huo kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo mkoani humo kabla hawajaondoka.

“Mkoa wetu wa Mwanza umejaliwa kuwa na vivutio vya aina mbalimbali na vya kipekee vya utalii ikiwa ni pamoja na fukwe nzuri zilizopo katika ziwa Viktoria, utalii wa majini, hifadhi ya taifa ya kisiwa cha saa nane na vivutio vya utalii vya utamaduni vilivyopo katika makumbusho ya utamaduni ya wasukuma buchosa,”amefafanua na kuongeza

“Pia Mkoa wetu wa Mwanza umezungukwa na visiwa, Wilaya ya Ukerewe tu inavisiwa takribani 38 visiwa vya ukerewe vina mambo mengi mazuri, kuna kisiwa  cha ukara ambacho kina jiwe linalocheza,”amebainisha Katibu Tawala Elikana.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi kwenye mkutano huo Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi sekta ya Miundombinu, Balozi Mhandisi Aisha Salim Amour ameielekeza Bodi ya Usajili wa Wahandisi nchini(ERB)kupeleka serikalini mpango mkakati utakaotatua changamoto za uhaba wa mafundi sanifu ikiwa ni pamoja na kuboresha mfumo wa elimu na ajira.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.