• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya awapa Rai Madaktari waliopata mafunzo maalum kwenda kuyafanyia kazi

Posted on: May 26th, 2023



Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana amewataka washiriki wa  mafunzo ya tathmini ya  ulemavu kwa ajali na magonjwa yatokanayo na kazi  kutumia vyema mafunzo waliyopatiwa na kuyafanyia kazi kwa vitendo.

Amesema hayo leo Mei 26, 2023 wakati akifunga mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Bima kwa Wafanyakazi (WCF) yaliyo wahusisha Madaktari 100 kutoka katika Mikoa ya kanda ya Ziwa ambayo yamefanyika Mkoani Kwanza.

"Nipende kutoa rai kwa washiriki wote kutumia vyema elimu iliyotolewa katika mafunzo haya ili kuwawezesha kufanya tathmini ya ulemavu kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu na hatimaye kuwasadia wanaopata ulemavu unaotokana na ajali au magonjwa yatokanayo na kazi na kuusaidia mfumo wa fidia kwa wafanyakazi kutimiza lengo la kutoa fidia stahiki na kwa wakati," amesema Mtendaji huyo wa Mkoa

"Nchi yetu na Dunia kwa ujumla imekumbwa na mabadiliko ya tabia nchi kutokana na uharibifu wa mazingira kwa msingi huo ni wajibu wa kila mmoja wetu kutunza na kuhifadhi mazingira yetu, tuchukue hatua za makusudi za kuhakikisha kuwa mazingira yetu yanalindwa ikiwemo kulinda vyanzo vya maji, misitu, na kuendelea na zoezi la upandaji miti katika maeneo yetu," ameongeza Ndg. Balandya.

Aidha Mkurugenzi wa Huduma na Tathmini wa (WCF) Dkt. Abdulsalaam Omar amesema mafunzo hayo kwa Madaktari yanakusudia kuusadia mfuko katika kufahamu asilimia za ulemavu na kutoa fidia stahiki na kwa wakati.

" Mafunzo haya yamejikita katika kuwawezesha madaktari kuweza kufanya tathmini lengo kwa ujumla ni kuongeza ufanisi wa kazi na kutoa huduma bora," amesema Dkt. Omar.

Naye Dkt. Paskalet Jumba mshiriki wa mafunzo kutoka Hospitali ya Rufaa Geita  amewasihi washiriki wenzie kwenda kuyafanyia kazi mafunzo waliyopatiwa pia  wanakwenda kuwaelemisha na wengine waliobaki katika vituo vya kazi ili waweze kuielewa elimu hiyo.

Mafunzo hayo  yameendeshwa kwa muda wa siku 5 ambayo yalifunguliwa Mei 22, 2023 na mpaka sasa Madaktari 1585 kwa Nchi nzima wamekwisha kupatiwa elimu hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.