• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AWAPONGEZA ICAP KWA USHIRIKIANO NA SERIKALI YA MKOA WA MWANZA

Posted on: November 12th, 2024

RAS BALANDYA AWAPONGEZA ICAP KWA USHIRIKIANO NA SERIKALI YA MKOA WA MWANZA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bwana Balandya Elikana leo Novemba 12, amewapokea na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirika lisilo la Kiserikali la ICAP kutoka nchini Marekani na kuwashukuru kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkoa wa Mwanza kwa kuwezesha ajira zaidi ya wafanyakazi 400 katika sekta ya afya.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea, Katibu Tawala amewashukuru Viongozi hao ambao ni Mkurugenzi wa Fedha wa ICAP kutoka Makao Makuu New York, Marekani, Bibi Amy Gustavsson, ambaye aliambatana na Naibu Mkurugenzi Mkazi wa ICAP Tanzania, Dkt. John Kahemele pamoja na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa shirika hilo nchini, Ndugu Godfrey Hoya kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha kinga dhidi ya kuzuia na matibabu ya Virusi vya UKIMWI Mkoani Mwanza.


Aidha Bwana Balandya amewashukuru kwa kuendelea kuhamasisha kutahiriwa kwa wanaume kwa hiari kati ya vijana wenye umri kuanzia miaka 18 mpaka 29, na ameshuhudia idadi kubwa ya vijana wakijitokeza kuhudhuria kliniki hiyo ambayo imekuwa na umuhimu mkubwa katika kupunguza maambukizi na kusambaa kwa virusi vya UKIMWI.

"Ninaendelea kuwashukuru kwani kupitia ICAP, Tumeongeza idadi ya wahudumu wa afya katika vituo vya afya ili kuhakikisha tuna rasilimali watu na tunafanikiwa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi".


Kadhalika amesema ushirikiano wa ICAP umesaidia katika ufungaji wa nishati ya jua kwenye vituo vya afya 81, hali iliyopelekea kuwepo kwa usambazaji wa umeme wa uhakika na huduma kutolewa bila adha ya nishati muhimu ya umeme.

Kwa upande wake, Bibi Amy amemshukuru Katibu Tawala na Serikali ya Tanzania kwa ujumla kwa ushirikiano mkubwa ambao ICAP imekuwa ikiupata na ameahidi kuendelea kushirikiana na Mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla ili kuboresha afya za wananchi na kufikia malengo ya kuimarisha huduma za afya nchini.

ICAP ni Shirika lililo chini ya Chuo Kikuu cha Columbia, linaendesha miradi mbalimbali ya afya Mkoani Mwanza inayolenga kupambana na UKIMWI na kifua kikuu kwa ufadhili wa serikali ya Marekani kupitia PEPFAR na CDC.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.