• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AWATAKA WATAALAMU WA MAABARA KUZINGATIA MISINGI YA TAALUMA

Posted on: September 25th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewasihi wataalamu wa Maabara nchini kuhakikisha wanazingatia msingi na kuwa na weledi wa kitaalamu wanapofanya uchunguzi na vipimo ili kupata matokeo sahihi na kupelekea matibabu halisi kwa wagonjwa.

Ametoa wito huo leo tarehe 25 Septemba, 2025 wakati akifungua Mkutano wa 38 wa Jumuiya ya Wataalamu wa Sayansi Maabara (MeLSAT) kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya nchini uliowakutanisha wataalamu zaidi ya 600 kutoka ndani na nje ya nchi katika Ukumbi wa Kwa Tunza Beach uliopo Ilemela mkoani Mwanza.

Amesema, ni lazima wanataaluma wa Sayansi ya Maabara kuhakikisha wanazingatia sheria za taaluma zao na kukiepusha na matendo ya rushwa na ubatili mwingine wowote ili kuhakikisha majibu ya uchunguzi yanakua halisi na kuweza kutoa matibabu yanayostahili kwa wagonjwa.

“Maabara ndio uti wa mgongo wa matibabu kwasababu kabla ya mgonjwa kupata tiba ni lazima afanyiwe uchunguzi na vipimo ndipo abainike anaumwa nini na kupatiwa tiba hivyo nawasihi mhakikishe mnakua kiungo bora cha matibabu nchini ili tupate taifa lenye watu wenye afya nzuri.” Amesisitiza Katibu Tawala.

Aidha, ametoa wito kwa wataaluma wa maabara kujiunga na kuzingatia katiba yao katika kulipa ada na kuwa wanachama hai ili ikiwezekana wanachama wote elfu 16 wawe katika mwamvuli mmoja tofauti na ilivyo sasa ambapo ni elfu 6 pekee wamejiunga na akatoa rai kwao kushiriki kwenye makongamano.

“Wana taaluma wote wa maabara naomba niwasihi, kama mnataka kufika mbali kwa pamoja ni lazima muwe wengi na wamoja hivyo nawaombe mjiunge kwenye chama chenu (MeLSAT) na waajiri nchini muwawezeshe kushiriki katika vikao vya kitaaluma kuanzia kwenye uandaaji wa bajeti.” Amesema, Balandya.

Raisi wa Chama hicho cha MeLSAT Bw. Yahya Mnung’a amesema wanachama katika kongamano hilo pamoja na mambo mengine watajadili changamoto na mafanikio ya taaluma yao na matumizi ya akili unde na athari zinazoweza kuathiri taaluma hiyo na kuweka mikakati ya kukabiliana na matokeo hasi ya teknolojia hiyo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.