• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Balandya: Wataalamu wa Kilimo tumieni mafunzo mnayopata ili mkalete mageuzi ya Kilimo- Biashara

Posted on: August 17th, 2023

RAS Balandya: Wataalamu wa Kilimo tumieni mafunzo mnayopata ili mkalete mageuzi ya Kilimo- Biashara


Wataalamu wa Kilimo kutoka Mikoa saba wanaondelea kupata mafunzo rejea ya siku mbili Mkoani Mwanza namna ya kuimarisha usimamizi wa huduma za ugani, wametakiwa kuja na mageuzi chanya kwenye sekta ya Kilimo ili kuwa cha kibiashara zaidi.

Rai hiyo imetolewa leo kwenye ukumbi wa Mtakatifu Dominic na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo na kuwahimiza kutimiza malengo ya Serikali ya ukuaji wa asilimia 10 kwenye sekta hiyo Ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala, Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Bw.Daniel Machunda amebainisha Serikali ya awamu ya sita imenuia kufanya mageuzi ya Kilimo kwa kutenga fedha nyingi za kuimarisha maeneo yote muhimu ikiwemo nyenzo za usafiri kwa Maafisa ugani.

"Kupitia agenda 10/30 azma ya Serikali ni kuongeza matumizi ya Teknolojia bora za kisasa ikiwemo matumizi sahihi ya pembejeo, kupima afya ya udongo na kuboresha miundombinu ya umwagiliaji." Machunda

Amewataka wataalamu hao kutumia kikamilifu siku za mafunzo hayo kwa kujadili namna ya kutoa huduma bora za ugani kwa wakulima na wadau wengine katika mnyororo wa thamani ili kuchangia katika kufikia malengo ya kitaifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa huduma za ugani kutoka Wizara ya Kilimo,Bi Upendo Mndeme amesema kuimarisha kwa huduma za ugani ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa kuendelezwa sekta ya kilimo (ASDP 2) ya kuongeza uzalishaji na tija.

"Ni lazima sasa tutoke kwenye kilimo cha kujikimu na kwenda kilimo biashara na kumfanya huyu mkulima kupiga hatua zaidi kwenye sekta hii ndiyo maana Serikali inahakikisha inafanya jitihada zote hizo kwa vitendo kwa kufanya uwekezaji mkubwa ili kilimo kipunguze umasikini na kujenga uchumi imara," amesisitiza Mndeme.

"Ndugu mgeni rasmi tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa kuonesha dhamira ya kweli ya kujenga uchumi imara kupitia sekta hii ya Kilimo,wajibu wetu sisi kama viongozi tuliopewa jukumu la kusimamia ni kuhakikisha malengo ya Serikali yanafikiwa kwa kufanya ufuatiliaji na  wakulima wanapata ushauri kwa wakati,"Emil Kasagara Katibu Tawala Msaidizi,Uchumi na Uzalisalhaji.

Kasagara amebainisha licha ya Wizara ya Kilimo kuwawezesha vyombo vya usafiri Maafisa ugani,imeanzisha mfumo wa kidigitali wa M-Kilimo ambao unamuwezesha mkulima kutumia simu za kiganjani kuwasiliana na maagmfusa ugani.

"Teknolojia ya M-Kilimo inawawezesha wakulima kupata ushauri kwa haraka na taarifa za masoko ya mazao ya Kilimo kwa njia ya simu za mkononi,hivyo kupitia mafunzo haya ni wajibu wenu Maafisa ugani kuwafundisha wakulima kutumia mfumo huu ili wapate huduma hizo,"Dkt.Rehema Mdendemi,mwakilishi kutoka TAMISEMI.

Wataalamu hao kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri wanatoka Mikoa ya Mwanza,Mara,Geita,Kigoma,Kagera,Shinyanga na Simiyu.

Kauli Mbiu ya mafunzo hayo ni "Agenda 1030 Kilimo-Biashata".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.