• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza afanya ukaguzi wa miradi ya afya isiyokamilika Sengerema,ataka taarifa ya mchakato wa ukamilishaji wiki hii

Posted on: December 19th, 2023

RAS Mwanza afanya ukaguzi wa miradi ya afya isiyokamilika Sengerema,ataka taarifa ya mchakato wa ukamilishaji wiki hii


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana ametoa maagizo ya kupatiwa  taarifa  ndani ya siku mbili kuhusu mchakato wa ukamilishaji wa miradi 17  ya afya wilayani Sengerema iliyojengwa kwa nguvu ya wananchi ili hatua za haraka zifanyike wananchi wapate huduma.

Akizungumza jana jumatatu na watendaji wa Halmashauri ya hiyo baada ya kufanya ukaguzi wa miradi iliyo kwenye vijiji tofauti, Balandya ameagiza kupatiwa gharama za umaliziaji zikiwemo na nyumba za watumishi na upatikanaji wa vifaa tiba.

"Mkurugenzi nimeona miradi ya zahanati imeishia hatua ya boma,

kaa na timu yako ya wataalamu mfanye kazi hii kwa umakini na taarifa niipate Ofisini kwangu  kabla ya jumatano ili ifanyiwe kazi ngazi husika," amesema Balandya wakati akiwa kijiji cha Nyamasale iliyopo zahanati iliyoishia hatua ya boma.

Akiwa kwenye kijiji cha Nyitundu iliyopo zahanati inayotoa huduma lakini inakabiliwa na uhaba wa vifaa tiba,nyumba za watumishi na wafanyakazi, Mtendaji huyo wa mkoa amemtaka Mkurugenzi kupatia ufumbuzi haraka wa changamoto hizo ili wananchi wapate huduma bora.

Balandya akiwa kwenye ukaguzi huo kijiji cha Tabaruka ameshuhudia  mradi wa zahanati uliofikia hatua ya ujenzi asilimia 38 huku zahanati ya kijiji cha Itonga ikitoa huduma lakini ikikabiliwa na uhaba wa maji na choo hakijakamilika, hapo ametoa agizo la kuchimbwa kisima haraka na ukamilishaji wa choo.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza imechukua hatua hiyo ikiwa ni utekekezaji wa maagizo ya Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa baada ya kufanya ukaguzi wa baadhi ya miradi hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita na kubaini mapungufu kadhaa, hata hivyo taarifa ya miradi 17 ya afya aliyopatiwa na mbunge wa Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu kuwa imekamilika lakini haitoi huduma haikuwa sahihi baada ya Katibu Tawala wa mkoa kubaini miradi hiyo bado ipo hatua ya awali kabisa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.