• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maafisa Ushirika Mwanza watakiwa kutumia Pikipiki walizokabidhiwa kwa malengo yaliyokusudiwa

Posted on: June 24th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike amewataka Maafisa Ushirika kutoka Halmashauri 5 za Mkoa huo aliowakabidhi Pikipiki zikatumike kama zilivyokusudiwa na kuleta matokeo chanya.

Akizungumza kwa niaba yake katika hafla fupi ya makabidhiano yaliyofanyika leo nje ya Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Joachim Otaru amesema Serikali kwa kutambua changamoto za utendaji kazi likiwemo suala la usafiri imewapatia usafiri huo hivyo jukumu lao ni kwenda kufanya kazi kwa Weledi.


"Serikali ya Awamu ya Sita ni sikivu imesikiliza changamoto zenu na kuzitatua kwa kuwapatia Pikipiki hizi sitarajii kuona mkizigeuza kama miradi ya kuwapatia vipato tofauti na hapo hatua za kinidhamu zitawahusu" Otaru

Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Mkoani Mwanza Lucas Kiondele amesema Maafisa Ushirika kwa muda mrefu wameshindwa kutekeleza ipasavyo majukumu yao ya kutoa elimu kutokana na umbali wa sehemu wanazotakiwa kwenda kufanya kazi, hivyo usafiri huo utaleta ufanisi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara amesema hizo ni hatua zinazofanywa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan katika jitihada za kuwaletea Maendeleo Wananchi, ametoa Pikipiki  pia kwa Maafisa Kilimo na Uvuvi.

Pikipiki hizo zimetolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa Maafisa Ushirika kutoka Halmashauri za Magu, Misungwi, Kwimba, Sengerema na Ukerewe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.