• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza awataka Wataalamu wa afya kuleta mageuzi chanya ndani ya Sekta hiyo

Posted on: July 22nd, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike amewataka Wataalamu wa Afya kutoka Halmashauri zote   Mkoani humo kuleta Mageuzi chanya kwenye Sekta hiyo hasa suala zima la Afya ya mama na mtoto.

Akifungua Kikao kazi cha Wataalamu hao cha Wilayani Sengerema walichokutana kujadili changamoto na kupanga mbinu bora za kuboresha afya ya mama na mtoto, Samike amesema bado kunahitajika uwajibikaji wenye Weledi katika kuboresha huduma ya afya kwa ujumla.

"Kila mwaka mnakuwa na vikao vya namna hii kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo lakini nikiangalia takwimu za mabadiliko hayaridhishi hasa suala la vifo vya mama na mtoto, anzeni kubadilika" amesisitiza Katibu Tawala.

Amewakumbusha Waganga Wakuu wa Wilaya kutumia muda mwingi kuzungukia kwenye Vituo vya Afya na kuzitatua changamoto zilizopo kwani kwa kufanya hivyo kutaongeza ari ya uwajibikaji kwa Watumishi wengine.

Ndugu Samike ameishukuru pia Serikali ya awamu ya Sita kwa kuendelea kujenga ushirikiano mzuri na Taasisi zisizo za Kiserikali ambazo zimekuwa zikitoa mchango katika Miradi mingi ya afya Mkoani Mwanza.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesema atasimamia na kutekeleza maagizo yote yanayolenga kutatua changamoto katika Sekta ya afya mkoani humo.

Kikao hicho cha siku 3 cha kupanga mfumo wa Afya ya uzazi kinaratibiwa na Shirika la USAID AFYA YANGU huku kikiwajumuisha watalaamu wa afya kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa, Waganga Wakuu wa Wilaya na Waratibu wa afya kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.