• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AZINDUA RASMI KAMBI YA MADAKTARI BINGWA BOBEZI HOSPITALI YA SEKOU TOURE

Posted on: October 28th, 2024

RAS MWANZA AZINDUA RASMI KAMBI YA MADAKTARI BINGWA BOBEZI HOSPITALI YA SEKOU TOURE


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Balandya Elikana amezindua rasmi kambi ya siku tano ya Madaktari bingwa bobezi wa moyo na huduma ya tiba kwenye hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mwanza-Sekou Toure na kuwahimiza wananchi wote kuchangamkia fursa hiyo ya matibabu.

Akizungumza leo Oktoba 28, 2024 na wananchi waliofika kwenye uzinduzi huo uliofanyika hospitalini hapo, Balandya amesema bado takwimu zinaonesha magonjwa yasiyoambukiza yanazidi kuongezeka ukiwemo shinikizo la damu ambao umeshika nafasi ya kwanza miongoni mwa magonjwa kumi.

"Zoezi hili ni muhimu sana kwetu sisi na tuzidi kupeleka taarifa kwa wananchi ili wafike kwa wingi kupata matibabu na ushauri pia, tusisubiri hadi hali iwe mbaya ni vizuri kujiangalia afya zetu mapema na kuanza matibabu," amesisitiza mtendaji huyo wa Mkoa.

Aidha, ameishukuru Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kuwaleta wataalamu hao na kutoa huduma hiyo Ijulikanayo kama "Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan Outreach Service" ambayo inasaidia kuimarisha afya za wananchi na hasa kwa kipindi hichi ambapo magonjwa yasiyoambukiza yanavyozidi kushika kasi.

Balandya pia ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuonesha kwa vitendo mkakati wa kuiboresha hospitali ya Sekou Toure ambayo inawahudumia wananchi zaidi ya milioni 3.

"Kambi hii ya siku tano tunatarajia kuleta matokeo chanya kwa wananchi wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo na mengineyo na hasa ambao wanaishi pasipo kujielewa changamoto zao za afya". Dkt.Jessica Lebba, Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya Sekou Toure, Bahati Msaki amebainisha kambi hiyo imeanza leo hadi Novemba Mosi mwaka huu na baada ya hapo matibabu kama hayo yataendelea hospitalini hapo kwani wapo madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali yakiwemo yasiyoambukiza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.