• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AZITAKA NGOs KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUONDOA WATOTO WA MTAANI

Posted on: January 27th, 2025

RAS MWANZA AZITAKA NGOs KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUONDOA WATOTO WA MTAANI


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana ameyataka Mashirika yasiyo ya Serikali Mkoani humo kushirikiana na Serikali kuwaondoa watoto wa mtaani kwa kuwapa elimu na kuwawezesha kubadili mtazamo wa maisha.

Ametoa wito huo leo tarehe 27 Januari, 2025 wakati akifungua Mkutano wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali zaidi ya 600 yanayofanya kazi mkoani humo yaliyoketi kwa utambulisho na kuwasilisha hali ya utekelezaji wa shughuli zao.

"Inawekezana pamoja na sababu zingine watoto wa mtaani wanasababishwa pia na ongezeko la watu kwani Mwanza ina muingiliano mkubwa wa watu hadi kufikia idadi ya milioni 3.6 hadi 4, hivyo tunapaswa kuhakikisha tunaitumia ardhi vizuri." Amesema Balandya.

Ameongeza kuwa, sekta ya uvuvi ina fursa nyingi za kuinua kiuchumi jamii mathalani ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa ya vizimba hivyo NGOs zihusishe jamii katika kuchakata chakula, kuzalisha vifaranga na hatimaye kuwa na ufugaji wa kisasa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini Bi. Mwamtumu Mahiza, amesema kuwa Serikali inachukua juhudi za makusudi kutambua changamoto za wadau hao ili kuwasaidia waweze kukidhi vigezo vya kusajiliwa na kuenenda vyema katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu ya sheria.

"Kwenye orodha nikiletewa taarifa nakuta mashirika zaidi ya elfu 10 lakini kwenye mfumo hawafiki elfu 4 na kwa hapa Mwanza ni miongoni mwa sehemu yenye shida hiyo maana naambiwa kuna mashirika zaidi ya 654 lakini 116 tu ndio wanalipa ada, tujirekebishe jamani." Bi. Mahiza.

Ameongeza kuwa NGOs hususani zinazojihusisha na Afya zinapaswa kufanya kazi kwa uzalendo kwa kulinda utamaduni, silka na utu wa nchi na sio kutoa taarifa za uongo ili kupata fedha za ufadhili mathalani kwenye taarifa za maambukizi na milipuko ya magonjwa nchini.

"Sisi NGOs bado tuna shida pamoja na kuwezeshwa na Serikali bado kiwango cha kuwajibika kwa mujibu wa sheria kiko chini kama vile usajiri na kulipa ada za uanachama kila mwaka na kufanya kazi kwa mujibu wa sheria hatuko vizuri ni lazima tujirekebishe." Amesema Gaspar Makala, Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali ..

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.