• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC atoa siku 20 kituo cha Afya Maisome -Buchosa kiwe kimekamilika

Posted on: February 28th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ametoa siku 20 kwa Mafundi wanaojenga Kituo cha Afya cha Maisome kukamilisha Ujenzi wa Majengo ya Mapokezi ya wagonjwa OPD na Maabadara ili huduma za afya zianze kutolewa.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo mapema leo kwenye Kisiwa hicho kilichopo kata ya Maisome-Buchosa wilayani Sengerema alipofika kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa kituo hicho pamoja na nyumba ya watumishi ambavyo Mwaka 2021 walipokea jumla ya Shilingi Milioni 250 kutoka Serikali kuu kupitia chanzo cha Tozo za Miamala ya Simu.

Amesema, kisiwa hicho chenye zaidi ya wananchi Elfu Ishirini kinapaswa kupata huduma za Afya zilizokamilika kwani wananchi wako mbali na maeneo mengine yenye huduma za Afya na hilo ndio lengo la Serikali kuleta fedha hizo lakini usimamizi umekua dhaifu na kusababisha ucheleweshaji.

"Wananchi zaidi ya Elfu Ishirini wa kisiwa hichi (Maisome) wamecheleweshwa kupata huda za Afya kwa zaidi ya Mwaka mmoja kutokana na usimamizi dhaifu kwenye Ujenzi huu, sasa nawapa siku 20 kufukia tarehe 19 Machi, 2023 muwe mmemaliza kujenga ili huduma zitolewe" Amesema Malima.

Katika hatua ingine, Mkuu wa Mkoa amewaagiza TAKUKURU kuupitia mradi huo ili ilikujiridhisha ni kwanini fedha zilizotengwa kujenga Kituo hicho hazikutosha hadi Halmashauri kuongeza Shilingi Milioni 30 kutoka mapato ya ndani na bado kuna malalamiko ya madai kwa mafundi wanaojenga mradi huo.

Vilevile, Mhe Malima ameitembelea shule pekee ya Sekondari kisiwani humo iitwayo Maisome na katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kujifunza ametoa ahadi ya kuwajengea Mabweni mawili kwenye shule hiyo ili kuwapunguzia umbali  wa zaidi ya Kilomita 12 wanafunzi wanaotoka vijiji vya mbali kama Busikimbi.

Akizungumza kwenye mkutano wa wananchi we kero, kiongozi huyo amemuagiza Mzabuni anayetoa huduma ya nishati ya umeme kisiwani humo kupunguza gharama za kila Uniti Moja utoka 3500 ili wananchi waweze kumudu na vilevile waongeze uwezo wa huduma uendane na mahitaji.

Mhe. Erick Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa ameahidi wananchi kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili wananchi wake kama kuboresha huduma ya Maji kwani tayari Rais Samia ameshawakabidhi Milioni 280 za kujenga miradi ya Maji na pamoja na ujenzi wa Barabara kuu ya kuongia jimboni humo kwa kiwango cha Changarawe.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amemshukuru Rais Samia kwa kuwahudumia wananchi kwa kuwapatia fedha za kutekeleza miradi mbalimbali na amemuahidi Mkuu wa Mkoa kutekeleza maagizo aliyoyatoa kwenye ziara yake aliyoifanya katika kuhakikisha wananchi wanaboreshewa mazingira

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.