• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Makalla afanya ukaguzi wa Jengo jipya la Abiria la uwanja wa ndege Mwanza,ahimiza ujenzi uendelee haraka

Posted on: May 30th, 2023

*RC Makalla afanya ukaguzi wa Jengo jipya la Abiria la uwanja wa ndege Mwanza,ahimiza ujenzi uendelee haraka


*Ataka TAA wakabidhiwe haraka mradi huo*


*Akiri kuwepo na Changamoto za kiujenzi



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Amos Makalla ameagiza mchakato wa makabidhiano wa Jengo jipya la Abiria la uwanja wa ndege kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwenda kwa Mamlaka ya viwanja vya ndege TAA ufanyike kwa haraka ili waendelee na kazi ya ujenzi.

Mhe.Makalla ametoa kauli leo mara baada ya kufanya ukaguzi wa Jengo hilo linalojengwa kwa kuchangiwa fedha kutoka Serikali kuu,Manispaa ya Ilemela na Jiji la Mwanza na kusisitiza hakuna sababu ya mradi huo kuendelea kusimama licha ya kuwepo na kasoro nyingi za kiufundi.

"Nimekuja kufanya ukaguzi wa Jengo hili mengi nitazungumza na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa,lakini nichukue nafasi hii kuhimiza TAA ndiyo wenye dhamana na jengo hilo hivyo waachiwe waendelee na ujenzi huu wakishirikiana na Wizara husika ya Ujenzi na Uchukuzi",CPA Makalla

Awali akitoa taarifa ya ujenzi huo ambao

 kwa sasa umesimama,Katibu Tawala Msaidizi,Miundombinu Mkoa wa Mwanza Mhandisi. Chagu Nghoma amesema Halmashauri ya Jiji la Mwanza wametoa zaidi ya Shs Bilioni 1.45,Ilemela zaidi ya Shs Bilioni 1.42 na Serikali kuu zaidi ya Shs Bilioni 9.

Aidha Afisa uendeshaji wa uwanja wa ndege Mwanza,Senneth Lyatuu aliyezungumza kwa niaba ya Meneja wa uwanja huo,amebainisha hawana utaratibu wa kuendesha shughuli zao kwa ubia na Taasisi nyingine za Serikali au Halmshauri.

Mhe Makalla ameshauri kuwepo na kikao baina ya pande zote husika zilizochangia fedha hizo ili kuona uwezekano wa kurudishiwa au taratibu nyingine.

Jengo la Abiria la uwanja wa ndege lilianza kujengwa mwaka 2019 kwa agizo la Rais wa awamu ya tano Hayati Dkt.John Magufuli kwa gharama ya zaidi ya Shs Bilioni 13 na hadi sasa zimetumika zaidi ya Shs Bilioni 9.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.