• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI

Posted on: May 31st, 2023

*RC MAKALLA AHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI*


*Aahidi kusimamia suala la Usalama kwa wananchi*


*Awataka Watumishi kuwa na nidhamu kazini, kutoa huduma bora*


*Ataka kuondoshwa kwa hoja za Ukaguzi na kutatua changamoto za ardhi*


*Awaagiza Sekta ya Maji kutatua kero ya upatikanaji wa huduma hiyo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Amos Makalla ametoa rai kwa Viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kushirikiana naye kwa dhati ili kutoa huduma bora na kuwaletea maendeleo wananchi.

Mhe. Makalla amesema hayo mapema leo Mei 31, 2023 wilayani Nyamagana wakati akizungumza na Viongozi, watendaji na  Makundi mbalimbali yakiwemo ya wanasiasa, wafanyabiashara na kamati ya Amani ya Wilaya hiyo kwa lengo la kujitambulisha rasmi.

Amesema ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora ni lazima watendaji na viongozi waliopewa dhamana ya kuhudumia wananchi kushirikiana kwa dhati na kufanya kazi kwa weledi ili kuwatatulia kero zao za kila siku wananchi.

Aidha, ameagiza ngazi zote za uongozi kuanzia ofisi za wenyeviti wa mitaa kusimamia suala la usalama wa wananchi wao ili kuwe na amani na kujenga ari ya kufanya kazi katika nyanja mbalimbali kwenye maeneo yao ikiwemo uvuvi, kilimo na biashara.

"Ipende kazi yako, fanya kazi kwa bidii, toa huduma bora kwa jamii na tukiwahudumia vema wananchi watakua na furaha kwani matatizo yao yatasililizwa na watahudumiwa vizuri, tukumbuke kuwa mwananchi akikosa huduma atailalamikia ofisi na sio wewe uliyemkwamisha kwa kujua tu haki bila wajibu." CPA Makalla akisisitiza juu ya uwajibikaji.

Vilevile, ameagiza Watumishi kujibu hoja za ukaguzi kwa wakati ili kuleta imani kwa wananchi na kwamba idara ya ardhi kujipanga kutimiza wajibu kwa kuzingatia matumizi bora ya ardhi na kutatua changamoto za ardhi kwa wananchi ili kuwa na mji uliopangiliwa vizuri.

"Moja ya maswali magumu ya Wananchi ni kwamba kwanini Mwanza iwe na shida ya Maji wakati ziwa lipo hapa jirani na huku wakiangalia Shinyanga wanapata maji kutoka hapa hivyo tuzuie upotevu wa maji kwani hiyo ni moja ya sifa mbaya sana kwahiyo lazima tuwe na mipango ya kutatua shida ya Maji kwa wananchi." Mhe. Makalla.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema kwa mwaka 2022/23 Halmashauri hiyo imekadiria kukusanya zaidi ya Shilingi Bilioni 23.6 na hadi  Aprili 2023 wamekusanya kwa ziaidi ya asilimia 75 ambapo ni ongezeko kubwa lilichagizwa na mipango kazi kabambe waliyojiwekea ukiwemo upangaji wa Wafanyabiashara kwenye maeneo rasmi.

Vilevile, amefafanua kuwa kutokana na mikakati waliyojiwekea ikiwemo kuwa na timu maalum ya Ukusanyaji wa mapato hadi kufikia mwishoni mwa  Juni mwaka huu Halmashauri ya jiji la Mwanza wanakusudia kufikia lengo na hata kuvuka ili kufanya vizuri kama mwaka uliopita ambao walikusanya Mapato ya ndani ya zaidi ya asilimia 105.

Aidha, Mhe. Makilagi amebainisha kuwa wamepokea fedha za Miradi ya Maendeleo kwa asilimia 77 kwani zaidi ya Shilingi Bilioni 79 zimepokelewa na kwa upande wa miradi ya kimkakati kama Meli ya MV Mwanza Bilioni 109, Ukarabati wa Meli ya MV Umoja  Bilioni 19 Stendi ya Mabasi ya Nyegezi Bilioni 18 na Soko kuu la Kisasa Bilioni 17 yote inaendelea vizuri kwani wakandarasi hawadai fedha na yote ipo hatua za ukamilishaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.