• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AMALIZA MGOGORO WA ENEO LA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI NYAMPULUKANO- SENGEREMA

Posted on: November 9th, 2023

RC MAKALLA AMALIZA MGOGORO WA ENEO LA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI NYAMPULUKANO- SENGEREMA


*Aaagiza ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Nyampulukano uanze kwa kasi kwani Serikali imetoa fedha Milioni 200*


*Aagiza pia shule mpya ya SEQUIP ujenzi uendelee haraka*


*Aagiza Mwezi Januari shule zote mpya zitakazojengwa zianze kutoa huduma*


*Awataka watendaji na viongozi kushirikiana  kuchapa kazi na kusahau msuguano wa nyuma*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amemaliza rasmi mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miezi sita wa wapi ujenzi wa shule mpya ya Sekondari chini ya Mradi wa Uboreshaji wa Elimu (SEQUIP) wapi ijengwe.

Mhe. Makalla ametatua mgogoro huo wakati akiongea na wananchi wa kata ya Nyampulukano eneo la FDC mlimani ambapo kabla ya kufika hapo alitembelea maeneo yote mawili yaliyopendekezwa kujengwa kwa shule hiyo mpya ya SEQUIP.

Mkuu wa mkoa amesema, kutokana na mgogoro huo kudumu kwa muda mrefu, Serikali ya awamu ya sita imeona ni vyema kujenga shule mpya katika maeneo yote mawili ya Misheni na Nyampulukano ili huduma hiyo muhimu iwafikie wote.

"Serikali imetoa shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha Miundombinu ya madarasa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi wakati huohuo shule mpya ya SEQIP itaendelea kujengwa katika eneo lililopendekezwa la kata ya Nyampulukano." Makalla.

Vilevile, amewataka Halmashauri ya wilaya ya sengerema kuongeza kasi ya ujenzi wa shule hizo na kwa pamoja ifikapo mwezi Januari mwakani zianze kutoa huduma kwa wananchi kwani wamesubiri kwa muda mrefu.

"Mimi kama Mtendaji mkuu nakusbukuru sana Mhe. Mkuu wa mkoa maana tulishakwama kutokana na sintofahamu ya wapi tutajenga shule pamoja na kupokea fedha za ujenzi huo, nakuahidi mwezi Januari shule hii itaanza na sasa tunafanya kazi kwa kasi", amesema Mkurugenzi Mtendaji, Binuru Shekidele.

Naye, Diwani kata ya Misheni Mhe. Francis Majumba amefafanua kuwa wananchi wa kata hiyo imepata faraja kutokana na kutatuliwa kwa kitendawili hicho na kupatikana kwa suluhu ambayo inakuja kuwatatulia adha ya kusuasua kwenye maendeleo kwenye eneo la Elimu.

Mapema asubuhi Mkuu wa Mkoa aliliagiza Shirika la Umeme wilaya Sengerema (TANESCO) kupeleka umeme kwenye shule mpya ya msingi ya Kijiweni iliyojengwa kwa zaidi ya shilingi Milioni 540 kwenye kata ya Chifunfu ambayo inakuja kuondoa kero ya msongamano wa wanafunzi kwenye shule mama ya Bugumbikiso.

Vilevile, amemtaka Mkandarasi anayejenga jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Sengerema kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwezi Mei 2024 kwa mujibu wa mkataba ili huduma zianze kutolewa hapo.

Halikadhalika, amewakaribisha wananchi wa wilaya hiyo kupata huduma za afya zinazotolewa kwenye hospitali mpya ya wilaya hiyo iliyojengwa kwa zaidi ya Bilioni 2.8 na ameahidi kuwasiliana na mamlaka husika ili ziletwe Bilioni 1.5 za kukamilisha ujenzi kwenye hospitali hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.