• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA APONGEZA UBORESHWAJI WA BANDARI NA KUWA MKOMBOZI KUPITIA MRADI WA SGR, MIZIGO MINGI KUFIKA KWA HARAKA MWANZA

Posted on: August 2nd, 2023

RC MAKALLA APONGEZA UBORESHWAJI WA BANDARI NA KUWA MKOMBOZI KUPITIA MRADI WA SGR, MIZIGO MINGI KUFIKA KWA HARAKA MWANZA


*Apongeza mpango wa uboreshwaji Bandari ya Dar utainua uchumi wa Mwanza kupitia mradi wa SGR


*Asema Fela ndiyo kituo Kikuu kitakachokuwa na shughuli nyingi za ushushaji mizigo na abiria,awataka wananchi kuchangamkia fursa za kiuchumi


*Awaondoa shaka wakazi wa kipande cha Fela kuja mjini fidia ya malipo yao kupisha mradi kulipwa mwezi huu


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla amepongeza uboreshwaji wa huduma ya Bandari ya Dar kuwa utainua uchumi wa Mkoa wa Mwanza kupitia mradi wa Treni iendayo kasi SGR kutokana na mizigo mingi kufika kwa haraka.

Akizungumza leo eneo la Fela na uongozi wa Kampuni ya CCECC pamoja na uongozi kutoka Wilaya ya Misungwi,.Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya kupatiwa taarifa ya awali akiwa ofisini kuhusu mradi huo amelazimika kuja kujionea maendeleo yake na amefurahi kazi nzuri ya Mkandarasi huyo.

"Mwanza ni Mkoa uliokaa kimkakati uliopakana na nchi za Maziwa makuu, ujenzi wa reli hii na uboreshwaji wa Bandari yetu hii ina maana wafanyabiashara watanufaika na kufanya shughuli zao kwa uhakika kutokana na mizigo yao kufika kwa usalama na haraka",CPA Makalla

Amewataka wananchi wa  Mwanza na hasa wakazi wa Wilaya ya Misungwi kumuunga mkono Rais Samia Suluhu na mkakati wa kuiboresha Bandari kwani ni faida kwao kiuchumi mara mradi huo wa SGR utakapo kamilika

Aidha amempongeza mkandarasi huyo Kampuni ya CCECC kutoka China  kwa kazi nzuri ya kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza na ana imani hadi kufika Mei mwakani ujenzi huo utakuwa umekamilika.

"Huu mradi kutoka Isaka hadi Mwanza wa KM 341 umegharimu Shs Trilioni 3 ni fedha nyingi na tunamshukuru Rais wetu kwa ahadi aliyoitoa ya kuiendeleza kikamilifu miradi yote ya kimkakati iliyowachwa na mtangulizi wake wa awamu ya tano Hayati John Magufuli,"amesema CPA Makalla.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa mradi wetu wa kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza tunaendelea vizuri na tumefikia asilimia 35 hadi sasa, licha ya changamoto ndogo ndogo za kiujenzi kama kuhamisha udongo na kuweka mwingine utakaomudu uzito wa mataluma tunakuahidi hadi kufika Mei mwakani tutakuwa tumeukamilisha," amefafanua Mhandisi Christopher Kalisti,Meneja wa mradi

Akiwa njiani kukagua mradi huo wa SGR Mhe.Makalla amesimama eneo la Mkuyuni Tambukareli na kupata wasaa wa kuzungumza na wananchi ambao wametoa maeneo yao kupisha mradi huo na kuwaondoa shaka kuhusu malipo ya fidia zao ambayo yatafanywa mwezi huu baada ya taratibu zote za msingi kukamilika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.