• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA MWANZA.

Posted on: October 13th, 2023

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI JIJI LA MWANZA


*Awataka watumishi wa Idara ya Ardhi kubadilika na kushughulikia kero za wananchi mapema*


*Ameliagiza Jiji la Mwanza kuhakiki na kulipa fidia kwa maeneo yaliyotwaliwa na Serikali*


*Aagiza Halmashauri ya Jiji kuzingatia mpango kabambe wa Ujenzi*


*Ayataka makampuni ya Ulinzi kuzingatia sheria na kanuni kwa wanaowaajiri*


*Awaagiza watendaji wa Serikali kuwa wepesi kusikiliza wananchi wakati wote na kuwasaidia*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameanza ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kukagua miradi ya Maendeleo kwenye halmashauri zote za mkoa huo ambapo leo Oktoba 12, 2023 amewasikiliza wananchi wa Nyamagana kwa zaidi ya saa nane (8).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Makalla amewataka watumishi wa Idara ya Ardhi-Jiji la Mwanza kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake watatue changamoto za wananchi ili kuepusha migogoro.

Amesema, kukithiri kwa kero za ardhi katika mkutano wake ni ishara kwamba idara hiyo haifanyi kazi zake ipasavyo na kwamba jambo hilo limepelekea jamii kukosa Imani nao kwani kumekua na urasimu usio na lazima ambao umekua ukikwamisha kusonga mbele kwa sekta hiyo.

"Jiji la Mwanza lina migogoro mingi ambayo imechangiwa na watendaji wa idara hiyo kutotatua kero za wananchi na badala yake kunakua na urasimu kwenye kushughulikia, napenda niwaambie kwamba kwa sasa mambo hayo hayana nafasi nataka muende na falsafa ya kushughulikia kero." CPA Makalla.


Vilevile, Mhe. Makalla ameagiza kuhakikiwa kwa maeneo yaliyotwawaliwa na Serikali kama maeneo ya shule pamoja na vituo vya kutolea huduma za afya ili yalipwe fidia na kuwe na mpango wa kuhakiki na kulipa mara moja na sio kulimbikiza usuluhishi hadi kupelekea migogoro.


Aidha, amewaagiza jiji hilo kuzingatia mpango kabambe wa Ujenzi ili kuepusha athari za ujenzi holela na uchafuzi wa mji kwa kuruhusu mabadiriko yasiyostahili ambayo hupelekea ujenzi holela na kuharibu mandhari ya jiji hilo.


CPA Makalla ametumia pia wasaa huo kuwataka wamiliki wa makampuni ya ulinzi mkoani humo kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kuwa na ajira zinazozingatia sheria na kuepusha migogoro.


"Msiogope hii ni fursa yenu ya kuonana moja kwa moja na Mkuu wenu wa Mkoa, njoo eleza kero yako maana nimekuja kusikiliza na kutatua kero zenu na kuwashauri pia namna ya kuepuka migogoro, nafasi hiyo ipo njooni." CPA Makalla akiwakaribisha wananchi.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amemshukuru kwa kusikiliza wananchi wa wilaya hiyo na kutatua kero zao ikiwa ni wilaya ya kwanza ya usikilizaji wa kero na akamuahidi kuwa wataendelea kusikiliza wananchi na kuwaondolea adha.


Ziara ya usikilizaji kero za wananchi imekuja kufuatia uzinduzi rasmi wa ngazi ya Mkoa uliofanywa tarehe 18 Septemba, 2023 ambapo alisikiliza kero 78 na Mhe. Mkuu wa Mkoa akaahidi kufanya ziara kabambe ya kusikiliza wananchi kwenye wilaya zote ili kuwatatulia kero zao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.