• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAAGIZA MAAFISA UGANI KUWAFUNDISHA WAKULIMA KANUNI BORA ZA KILIMO

Posted on: August 8th, 2023

RC MAKALLA AWAAGIZA MAAFISA UGANI KUWAFUNDISHA WAKULIMA KANUNI BORA ZA KILIMO


*Awataka kuanzisha mashamba darasa kwenye maeneo yao*


*Awaasa Vijana kujikita kwenye Kilimo na Ufugaji wa Kisasa*


*Awataka vijana kuacha uvuvi haramu na kilimo cha mtandaoni*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ametoa rai kwa Maafisa Ugani wa Kanda ya Ziwa Magharibi kuwatembelea wakulima na wafugaji ili kuwakumbusha juu ya kuzingatia kanuni bora za kilimo na ufugaji ili kuweza kupata tija kubwa kwenye uzalishaji.

CPA Makalla ametoa rai hiyo leo tarehe 8 Agosti 2023 wakati akizungumza na wananchi wa Kanda ya Ziwa Magharibi katika kilele cha maonesho ya Wakulima (Nane Nane) yaliyowakutanisha kwa Siku 8 Mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza ambapo ameyafunga rasmi.

"Kwakua ninyi ni wataalamu na ndio kazi yenu msichoke kuwatembelea wakulima na wafugaji na kuwapa ushauri stahiki na katika maeneo yenu ya kazi anzisheni mashamba darasa ili wakulima waendelee kujifunza na kuyaona mafanikio." Amesisitiza.

Aidha, ametoa wito kwa vijana kuacha kufanya kilimo mtandaoni na uvuvi haramu badala yake amewataka kujikita kwenye kilimo na ufugaji wa kisasa wa samaki kwani Rais Samia amekua akitoa fedha nyingi kwenye kuwainua vijana kiuchumi kwa kuwapatia mikopo ya aina mbalimbali.

"Tafiti mbalimbali juu ya zao la pamba zinaonesha kwenye hekari moja mkulima anaweza kupata kilo 800 hadi 1200 wakati hali halisi ya mavuno kwa mkulima ni kati ya kilo 150 hadi 300 na kwa ng'ombe wa maziwa anaweza kufikia lita 25-30 kwa siku wakati hali halisi kwa sasa lita 10 kwa ng'ombe". Mhe. Makalla.

Vilevile, amebainisha kuwa Mkoa wa Mwanza katika msimu wa 2022/23 ulihekta 455,498.05 na kuzalisha tani 634,373.78 sawa na asilimia 80 hadi kufikia Juni na akabainisha kuwa elimu waliyoipata hapo itawasaidia kufanya mageuzi katika sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji

kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Emil Kasagara amefafanua kuwa maonesho hayo yamewapa fursa wadau kutoka sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambazo huhusisha Utafiti, Umwagiliaji pamoja na hifadhi za Mazao kujifunza kwa vitendo.

"Katika maonesho ya kilimo na sherehe za Wakulima (Nane nane) 2023 jumla ya wadau 863 wameshiriki. Idadi hii inajumuisha Mamlaka za Serikali za Mitaa13, Taasisi za Serikali 11, Taasisi za Fedha 07, Taasisi za Elimu 10, Makampuni ya zana za kilimo 09 pamoja na wajasiriamali wakubwa na wadogo 746." Kasagara.

Maadhimisho hayo ya 2023 yameenda sambamba na kaulimbiu: "Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula."

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.