• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAKARIBISHA INDONESIA KUWEKEZA MAZAO YA NGOZI NA MADINI

Posted on: February 26th, 2024

RC MAKALLA AWAKARIBISHA INDONESIA KUWEKEZA MAZAO YA NGOZI NA MADINI


*Asema Mwanza ina maeneo mengi yenye fursa za uwekezaji ukiwemo uvuvi


*Apongeza uhusiano wa Tanzania na Indonesia ulioanza tangu mwaka 1964


*Asema makubaliano ya mashirikiano yaliyofanywa na Marais yataongeza tija ya Maendeleo*


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo amefanya mazungumzo mafupi na Balozi wa Indonesia hapa nchini Mhe.Tri Yogo Jatmiko na kutoa fursa ya kuwekeza katika mazao ya ngozi na madini yanayopatikana kwa wingi mkoani humo.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa yakijumuisha maafisa kutoka ubalozi huo na mwakilishi kutoka Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkuu huyo wa mkoa amesema makubaliano ya mashirikiano  yaliyofanywa na viongozi wa Mataifa hayo hivi karibuni ni lazima yawe na matokeo chanya kama uwekezaji huo.

"Mhe Rais wetu alifanya ziara hivi karibuni nchini Indonesia na kuingia makubaliano ya mashirikiano katika sekta mbalimbali kama elimu,kilimo,afya na biashara,lakini pia hapa mkoani kwetu zipo fursa nyingi ambazo zikipata mwekezaji zitakuwa na tija kwa wananchi wa pande zote mbili,"CPA Makalla

Amebainisha nchi ya Indonesia tuliyoingia nayo mahusiano tangu mwaka 1964 ni wazalishaji wakubwa wa mafuta ya mawese ambayo waliyatoa hapa nchini kwetu, wamewekeza zao la karafuu huko Zanzibar na sasa wanataka kujikita kwenye zao la Tangawizi,hii yote ni faida ya ushirikiano mzuri uliopo baina ya nchi hizo.

Aisha ameipongeza Indonesia kwa kuwajengea uwezo wataalam wa chuo cha DIT hali ambayo itaongeza tija Katika uzalishaji bora wa mazao ya ngozi.


Naye Balozi wa Indonesia Tri Yogo Jatmiko amesema anatekeleza na kuimarisha makubaliano yaliyowekwa baina ya nchi ya Indonesia na Tanzania katika sekta mbalimbali.

Indonesia imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam wa ngozi kwenye chuo cha DIT kuanzia leo hadi Machi 8 2024 na mafunzo hayo yatakuwa yakifanyika kwa awamu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.