• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI MWANZA

Posted on: November 3rd, 2023

RC MAKALLA AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI MWANZA


Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masalla amewakaribisha wafanyabiashara kuchangamkia fursa za uwekezaji mkoani Mwanza kutokana na kuwepo na mazingira rafiki ya kuwekeza.

Akizungumza leo Novemba 3, 2023 kwa niaba ya Mkuu wa Mko kwenye kongamano la kibiashara la Jiongeze lililoandaliwa na Kampuni ya Wasafi, Mhe.Masalla amesema kukamilika kwa miradi ya kimkakati ikiwemo Reli ya kisasa SGR,Daraja la JP Magufuli na Meli ya abiria ya Mv Mwanza zitachangia kurahisisha shughuli zote za kibiashara.

"Mwanza tuna rasilimali kubwa ya Ziwa Victoria kunakofanyika shughuli za uvuvi wa samaki na dagaa utakapo wekeza eneo hili utakuwa na uhakika wa kipato kutokana na miundombinu ya usafirishaji kuwa rafiki iwe barabara,ndege au njia ya reli,"amesisitiza Mkuu huyo wa Wilaya akizungumza na washiriki wa kongamano hilo.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara wengi walishindwa kusafirisha mizigo yao kwa ukubwa lakini kuwepo kwa mradi wa reli ya kisasa na uwepo wa Meli uhakika wa kusafirisha mizigo kwa usalama na kwa wingi sasa hakuna shaka.

Awali akitoa utangulizi wa taarifa za fursa za uwekezaji Mwanza,Katibu Tawala wa Mkoa huo,Ndg.Balandya Elikana amebainisha Mkoa huo kuwa karibu na eneo la nchi za maziwa makuu ni fursa pekee ya kiuchumi kutokana na mazingira rafiki ya miundombinu ya usafiri.

"Ukuaji wa kiuchumi wa Mkoa wa Mwanza ni lazima sasa bidhaa nyingi zipatikane hapa tofauti na wengi kukimbilia Kariakoo,uwanja wetu wa ndege upo mbioni kukamilika na kuwa wa kimataifa Utalii utakuwa na tija kutokana na ukaribu wa Mwanza na mbuga ya Serengeti ambao ni mwendo wa saa mbili na nusu,"Balandya.

Kongamano hilo lililokuwa na utoaji wa mada mbalimbali kutoka kwa wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Taasisi za Serikali,washiriki walipata fursa ya kujua ufugaji wa kisasa wa ng'ombe aina ya Borani.

"Tuna shamba letu la Taifa la Mabuki huko sasa hivi kunaendelea mradi wa utoaji elimu kwa vijana namna ya ufugaji wa ng'ombe kwa tija ikiwemo utoaji maziwa kwa wingi na unenepeshaji wa kuwa na kilo zaidi ya 200",Peter Kasele,Afisa mifugo.

"Mkoa wa Mwanza alisilimia 53 ni maji ya ziwa Victoria hivyo kilimo cha umwagiliaji kina nafasi kubwa,mazao ya jamii ya mikunde,mahindi pia mpunga kina stawi sana,"Innocent Keya, Afisa kilimo.

"Tuna vivutio vingi vya Utalii Mkoani Mwanza,kuanzia mbuga ya Sanane,makumbusho ya mila za kabila la wasukuma ya Bujora pamoja na Utalii ndani ya Ziwa Victoria hasa uwepo wa jiwe la Bismark,"Gloria Mnihambo,Afisa bodi ya Utalii.

Kongamano hilo limewajumuisha zaidi ya washiriki 200 kutoka maeneo mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara,wadau wa sekta ya Utalii,pamoja na wanafunzi kutoka baadhi ya vyuo vikuu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.