• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAPA KONGOLE NMB KWA KUWAUNGANISHA WATEJA KATIKA MFUMO RASMI WA KIFEDHA

Posted on: September 15th, 2023

RC MAKALLA AWAPA KONGOLE NMB KWA KUWAUNGANISHA WATEJA KATIKA MFUMO RASMI WA KIFEDHA


*Asema kuwajumuisha watanzania kwenye mfumo rasmi wa kifedha kunasaidia kuinua kipato*


*Aipongeza kwa kubuni bidhaa zinazolenga mahitaji ya kila kundi kwenye soko na kwa kutoa mikopo*


*Atoa wito kuandaa programu kwa watumishi wengine wa serikali*


*Atoa wito kwa walimu kuhifadhi pesa benki na kuachana na mikopo yenye masharti magumu*


CPA Amos Makalla ameipongeza benki ya NMB kwa kuwatunza walimu kwa masuluhisho mbalimbali ya kifedha na kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwajumuisha watanzania katika mfumo rasmi wa kifedha ili kuinua vipato vyao na uchumi kwa ujumla.

Ametoa pongezi hizo leo tarehe 15 septemba, 2023 kwenye warsha ya siku ya walimu iliyoandaliwa na benki hiyo ambayo imezindua mpango wa kuwafikia walimu zaidi ya 9,000 kote nchini kwa kaulimbiu ya "Mwalimu Spesho- Umetufunza Tunakutunza."

 "Nimeambiwa kuwa madhumuni ya siku hii ni pamoja na kutambua mahusiano mazuri yaliyopo na kutoa fursa kwa walimu kutoa maoni na mapendekezo ya namna gani wanaweza kunufaika zaidi na huduma za benki hii, hakika jambo hili linatupa faraja sana  kwakweli naomba niwapongeze sana NMB." Mhe. Mkuu wa Mkoa.


"Jitihada hizi ni nzuri na zinaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya Sita katika kuhakikisha watanzania wanajumuishwa katika mfumo rasmi wa kifedha ili kuinua vipato vyao na uchumi kwa ujumla, natoa rai kwa mabenki na taasisi zingine za kifedha kuunga mkono ili elimu hii iwafikie wengi hasa maeneo ya vijijini." Amesisitiza Makalla.


Makalla amesema uamuzi wa kuwakutanisha walimu ni wa kizalendo na unafaa kuigwa na kila taasisi kwani unaonesha kuwajali walimu na utakuza mahusiano mazuri kati ya pande hizo mbili za benki na sekta ya elimu hapa nchini.


Vilevile, ametumia wasaa huo kuwapongeza kwa kubuni bidhaa zinazolenga mahitaji ya kila kundi kwenye soko na kwa kutoa mikopo mingi kwa wafanyakazi wa Serikali kuu na za mitaa ambapo asilimia kubwa ya walimu wananufaika nayo kwa kukidhi mahitaji ya familia na hata maandalizi ya maisha baada ya kustaafu.

"Nawasihi kuendelea kuandaa programu nyingi si kwa walimu tu hata kwa watumishi wengine wa Serikali ili kuwapa fursa ya kuongeza ufahamu wa huduma na muendelee kubuni huduma nafuu zaidi ambazo mfanyakazi wa kawaida anaweza kuzimudu." CPA. Makalla.

Aikansia Muro, Mkuu wa Idara ya wateja binafsi amesema kwa kipindi cha miaka 8 mfululizo wanakutana na walimu kwenye siku maalumu na makongamano hayo yamekua yakiwapa fursa kama wateja kuelimishwa juu ya huduma na inatoa nafasi kwa benki hiyo kupokea maoni juu ya huduma zao na kwenda kuziboresha.


"Benki ya NMB tutaendelea kuwa na masuluhisho bora ili kuwaleta watanzania pamoja na katika huduma bora za kifedha nchini, na tutaendelea kubuni huduma bora zaidi kwa ajili ya makundi yote nchini hata wafanyabiashara wadogo na wakulima." Bi. Aikansia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.