• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA WADAU MKOANI HUMO KUTOA MAONI YA KINA KWENYE DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Posted on: July 24th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WADAU MKOANI HUMO KUTOA MAONI YA KINA KWENYE DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050


*Azitaka Taasisi kuainisha Vipaumbele vya Bajeti na Maendeleo ya Jamii*


*Atoa wito kwa Sekta za Uvuvi, Kilimo cha Pamba na Uchimbaji wa Madini kushiriki kikamilifu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wadau Mkoani humo kushiriki vema katika kutoa Maoni ya Kitaalamu katika kuhakikisha wanachangia vema kwenye upatikanaji wa Dira Bora ya Maendeleo 2050.

Ametoa wito huo leo tarehe 24 Julai 2023 wakati akifungua Warsha ya Uelimishaji Umma juu ya uandaaji wa Dira ya Taifa 2050 iliyowakutanisha Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wilaya, Wakurugenzi, Wakuu wa Seksheni na Vitengo na Wakuu wa Taasisi mbalimbali.

Makalla amesema, katika kupanga malengo ya muda mrefu kama Dira ya Maendeleo ni lazima kila taasisi iainishe Vipaumbele, Bajeti na Maendeleo ya Jamii hivyo ni lazima kuthamini fursa waliyoipata ya kuwa sehemu ya kuchangia maoni na kuitumia vema.

"Ni kikao chetu muhimu sana katika kuelekea maendeleo endelevu ya miaka ya mbele mathalani jeshi la Polisi lazima liweze kupanga linataka liwe la aina gani kwa mfano kwenye kupambana na wizi wa kimtandao." CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amezitaka Sekta kuu za kiuchumi kama Uvuvi, Kilimo cha Pamba, Uchimbaji wa Madini kupanga vema kwenye vipaumbele mahususi vitakavyokuza sekta zao kiuchumi ili kusaidia wananchi walio wengi maana ndizo shughuli kuu za kiuchumi Mkoani humo.

"Taifa letu limekua na Dira ya Maendeleo ya kuishia 2025 na sasa Serikali ipo kwenye maandalizi ya dira kuelekea 2050 ambapo tumekutana makundi mbalimbali kwa kushirikiana na ngazi ya Taifa katika kuhakikisha kila kundi linahusika kwenye kutoa maoni." Amesema Katibu Tawala Mkoa, Balandya Elikana.

Bwana Omary Othman, Mjumbe wa Maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa amesema wanahamasisha na kutoa elimu ili kupata ufahamu wa pamoja na kwamba wanategemea viongozi wa Mkoa husika watapeleka elimu hiyo hadi chini ili wananchi waweze kushiriki vema kutoa maoni wakati wa zoezi hilo utakapofika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.