• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULILETEA TAIFA MAENDELEO

Posted on: March 16th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULILETEA TAIFA MAENDELEO


*Awaasa watumishi kuwa na weledi, bidii na wazalendo kwa Taifa*


*Ataka taarifa ya utekelezaji wa shughuli kutolewa katika kila robo*


*Baraza laipongeza Idara ya Utumishi RS Mwanza kwa kujali watumishi*


Mhe. Amina Makilagi, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana amewataka Watumishi na waajiri Mkoani Mwanza kutimiza wajibu wao wa kisheria wa kuwahi kazini, kutunza mali za umma na kuwa wazalendo ili kukuza utumishi kwa pamoja na kuliletea Taifa maendeleo.

Mhe. Makilagi amesema hayo leo Machi 16, 2024 wakati akilihutubia Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza lililofanyika kwenye Ukumbi wa Wag Hill Resort chini ya Kaulimbiu ya 'Tutatue Changamoto kwa Pamoja'.

Aidha, Mhe. Makilagi amesema mpango wa bajeti katika idara ni lazima uwe shirikishi kwa watumishi ili kila mmoja ajue ni shughuli gani itatekelezwa na kwa wakati gani, na sambamba na hilo akatoa wito kwa watumishi kutofuja fedha za umma na kuepuka rushwa mahala pa kazi.

Mwenyekiti wa baraza la Wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza Emily Kasagara ametoa wito kwa watumishi kushirikiana katika kutimiza Dira ya maendeleo ya miaka mitano na kufanya kazi kwa bidii, weledi, juhudi na kuwa wabunifu ili kujenga Taifa uchumi wa nchi.

"Hadi kufikia mwisho wa mwaka mwezi Juni, 2023 jumla ya Sh. 478,226, 133,790 zilipokelewa sawa na asilimia 96.6 ya fedha zote zilizoidhinishwa na kwamba hiyo ni sawa na asilimia 95 ya fedha zilizopokelewa," amefafanua Mkuu wa Seksheni ya Mipango na Uratibu Henry Mwaijega.


Mwaijega ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2023/24 Mkoa umeidhinishiwa kutumia zaidi ya Bilioni 487 na kwamba kumekua na ongezeko la Bilioni 16.8 sawa na asilimia 3.5 ikilinganishwa na 2022/23 huku ongezeko hilo likitokana na fedha za mishahara, matumizi mengineyo na fedha za miradi kutoka serikali kuu kuongezeka.

Halikadhalika, amewasilisha pia rasimu ya Bajeti ya Mkoa na Halmashauri zake kwa mwaka 2024/25 inayoonesha kuwa mkoa umepanga jumla ya Sh. 523, 067,403,641 kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake. zikijumuisha zaidi ya Bilioni 308 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Bilioni 142.5 kwa shughuli za maendeleo.


Akiwasilisha taarifa za kiutawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu Bi. Franciscar Mmari amesema hadi kufikia Disemba 2023 watumishi 25 wa kada mbalimbali walipandishwa vyeo huku 5 hawakupandishwa kutokana na kukosa sifa za muundo kwa mujibu wa miundo ya maendeleo ya utumishi wa kada zao.

Aidha, ametoa rai katika uandaaji wa ikama na bajeti ya mishahara uzingatie miundo ya maendeleo ya utumishi, miundo ya mshahara, mfumo wa usimamizi wa taarifa za kiutumishi na mishahara pamoja na bajeti kutengwa na kituo cha kazi husika na si vinginevyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.