• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZINDUA JENGO LA WAGONJWA WANAOHITAJI UANGALIZI MAALUM (ICU) BWISYA-UKARA

Posted on: November 22nd, 2023

RC MAKALLA AZINDUA JENGO LA WAGONJWA WANAOHITAJI UANGALIZI MAALUM (ICU) BWISYA-UKARA


*Lajengwa kwenye Hospitali yenye hadhi ya Wilaya Bwisya -Kisiwani Ukara*


*Awapongeza wasimamizi kwa kuokoa fedha zaidi ya Milioni 70 zilizojenga nyumba ya watumishi*


*Aagiza Ofisi ya Mganga Mkuu Mkoa kupanga ratiba za Madaktari bingwa kufika kwenye hospitali hiyo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla, leo Novemba 22, 2023 amezindua jengo la wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum lililojengwa kwenye Hospitali ya Bwisya kwenye kisiwa cha Ukara kwa Shilingi Milioni 177 kati ya 250 zilizotengwa.

Akiongea na watumishi na wananchi, CPA Makalla ameipongeza halmashauri ya Ukerewe kwa usimamizi mzuri wa mradi uliopelekea kuokoa fedha zaidi ya Milioni 70 ambazo zimesaidia kujenga nyumba ya watumishi ya familia tatu kwenye hospitali hiyo baada ya kuongeza milioni 30 kutoka kwenye mapato ya ndani.

Mhe. Makalla amesema Rais Samia amewaletea huduma hiyo karibu kwa upendo wake kwani awali wananchi waliokua wakihitaji huduma hizo walilazimika kusafiri kwenda kwenye kisiwa cha Nansio wilayani Ukerewe jambo ambalo lilihatarisha afya zao.

"Nimezunguka ndani ya jengo hili (ICU) na nimeona limejengwa katika viwango bora na limewekewa vifaa vya kisasa kwa mahitaji ya kutibu wagonjwa watakaokua kwenye hali mahututi hivyo naomba mvitunze na kero ya watumishi wachache ninakwenda kulifuatilia", amesema Makalla.

Halikadhalika, ametumia hafla hiyo kumuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa kupanga ratiba za Madaktari bingwa kutoka kwenye hospitali ya rufaa ya Kanda Bugando kufika kwenye hospitali hiyo kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa kwa wagonjwa kwani jiografia inawapa ugumu kuzifuata jijini Mwanza.

"Uchache wenu (watumishi) usiwapelekee mkatoa huduma hafifu, tuendelee kuhudumia wananchi kwa upendo nami kwa nafasi yangu nitafuatilia suala la watumishi kuletwa hapa." Amesema Mhe. Joseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kwa niaba ya wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.