• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZINDUA MAJARIBIO YA CHANZO KIPYA CHA MAJI BUTIMBA, HUDUMA YA MAJI MWANZA KUIMARIKA

Posted on: September 15th, 2023

RC MAKALLA AZINDUA MAJARIBIO YA CHANZO KIPYA CHA MAJI BUTIMBA, HUDUMA YA MAJI MWANZA KUIMARIKA


*Amshukuru Rais Samia kwa Kutoa zaidi ya Bilioni 69 za mradi huo*


*Atoa wito kwa Wabunge kufanya mikutano ya hadhara kuelezea uboreshaji mkubwa wa miradi ya Maji*


*Asema Mkandarasi wa kujenga mradi mwingine mkubwa kupatikana ndani ya muda mfupi*


*Awataka Wananchi kutoa taarifa MWAUWASA waonapo Maji yakivuja Mtaani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla leo Septemba 15, 2023 amezindua Majaribio ya Chanzo Kipya cha Tiba ya Maji Butimba kituo ambacho kitazalisha Lita milioni 48 kwa siku kilichojengwa na Kampuni ya Sogea Satom chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA).

Akizungumza na wananchi baada ya kubonyeza kitufe na kuwasha mitambo ya Maji na hivyo kuanzisha rasmi majaribio Mhe. Makalla amesema katika muda mfupi ujao wananchi wanaoishi katika maeneo ya Sahwa, Igoma, Kishiri, Nyamhongolo na Kisesa wataanza kupata Maji kutoka katika chanzo hicho kilichogharimu zaidi ya bilioni 69.


Mhe. Mkuu wa Mkoa ametumia hafla hiyo kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuendelea kutoa fedha ili kutekeleza mradi huo unaotarajia kuongeza uzalishaji hadi lita milioni 138 kwa siku kutokana na chanzo cha sasa kuzalisha lita milioni 90 na miradi mingine inayolenga kuondoa kero ya Maji kwa wananchi Mkoani humo na wataalamu wote waliofanikisha ujenzi wa mradi huo.

Vilevile, Mhe. Makalla amebainisha kwamba kupitia mradi wa LVWATSAN kwa suluhisho la muda wa kati tayari zabuni kwa ajili ya ujenzi wa mtandao wa mabomba na Matenki makubwa sita yenye uwezo wa kuhifadhi maji jumla ya Lita milioni 31 imetangazwa na kwamba mkandarasi anatarajiwa kupatikana siku za usoni.


"Ndugu wananchi, napenda kuchukua fursa hii kuwaomba mnapoona maji yakivuja mtaani mtoe taarifa MWAUWASA  nanyi mzishughulikie taarifa hizo kwa haraka na kwa umakini ili kuokoa maji, kuwatia moyo wananchi na kuzuia matatizo kama hayo yasijitokeze tena sehemu ileile." Mkuu wa Mkoa.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa, Mhe. Sixbert Gichabu amesema chama tawala kina matarajio makubwa kwa Serikali yao na Mhe. Rais Samia ameamua kuwaletea huduma bora wananchi na ametoa pongezi kwa MWAUWASA kwa kutoa elimu kwa umma kila wakati juu ya maendeleo ya huduma za maji.


Naye, Mbunge wa jimbo la Nyamagana Mhe. Stansilaus Mabula ametumia wasaa huo kutoa shukrani kwa Rais Samia kutokana na jitihada za kuwaletea wananchi wake Maji safi na Salama huku akibainisha kuwa Mhe. Rais aliahidi mwenyewe kumaliza tatizo la maji jijini humo.


"Pamoja na jitihada hizi, iko haja ya kufumua mifumo na kuangalia mabomba yanayosambaza maji kama yanakidhi uwezo na kufanya ukarabati mara moja ili Miundombinu iende sambamba na mahitaji na kwakweli tunamshukuru sana Mhe. Rais Samia kwa kuwajali wananchi." Mhe. Angelina Mabula, Mbunge wa Ilemela.


Kaimu Mkurugenzi MWAUWASA, Bi. Nelly Msuya amesema mahitaji ya Maji jijini mwanza ni zaidi ya lita Milioni 165 kwa siku na kwamba chanzo cha zamani ambacho kinahuumia sasa cha Kapripoint kimekua kikizalisha Lita milioni 90 tu kwa siku hivyo Serikali kuona umuhimu kuongeza miradi mingine ili kuongeza uzalishaji.

"Kwa mujibu wa Mkataba ifikapo  tarehe 30 mwezi Oktoba mwaka huu mradi huu utakabidhiwa rasmi na kuanza kutumika kwani hadi sasa umefikia asilimia 96 ya ujenzi na unatarajiwa kuboresha huduma hii muhimu kwani utaunganishwa kwenye mtandao wa mabomba ya zamani na mtandao mpya."Amesisitiza Bi. Nelly.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.