• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ahimiza wakandarasi Jengo la Abiria Uwanja wa Ndege Mwanza kulikamilisha kwa wakati

Posted on: September 28th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka wasimamizi wa Mradi wa Ujenzi wa jengo la kisasa la abiria kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza kusimamia kwa dhati na wawe na kiu ya kuukamilisha kwa wakati ili uanze kutumika.

Mhe. Malima amesema hayo leo wakati wa Kikao Kazi cha kujadili Mapendekezo Mapya ya Usanifu wa baadhi ya maeneo kwenye Jengo jipya la Abiria kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza ambapo amebainisha kuwa litakapokamilika jengo hilo la kisasa litasaidia kuinua uchumi kwenye ukanda huo.

"Ninachokitaka kwenu nyie Wahandisi, msimamie kwa uzalendo ujenzi huu na kila mmoja wetu hapa awe na lengo la kuukamilisha maana mradi huu ni wetu sote na utainua sana utalii wa nchi hasa kwenye ukanda wa kanda ya ziwa." Malima.

Amesema, Mkoa wa Mwanza unawekeza kwenye majengo hayo kwa kupitia Halmashauri za Manispaa ya Ilemela na Nyamagana zilizotoa fedha Tshs. Bilioni 4 za mapato ya ndani kwenye ujenzi huo na amewasihi kuongeza fedha ili likamilike na amefafanua kuwa litakapokamilika utawekwa utaratibu wa kuwa wadau wa uwekezaji ili kiasi fulani cha fedha zirudi kwenye Halmashauri hizo.

Katika kuimarisha uchumi wa Mwanza kupitia sekta ya Utalii, Malima ametoa mfano wa uzao wa Nyumbu unaofanyika kila mwaka mwezi februari kwenye hifadhi ya Serengeti kuwa jengo hilo litakapokamilika litatumika kwakua litakua maridadi na nadhifu kwa viwango vya ndani na nje ya nchi.

Mhe. Malima amesisitiza uzalendo kwenye ujenzi huo kwa kuzingatia bei ya manunuzi ya vifaa na kusimamia ubora wa jengo ili liweze kudumu kwa muda mrefu na kuwanufaisha wanachi wa mikoa ya kanda ya ziwa na Taifa kwa ujumla.

Ndugu Balandya Elikana, Katibu Tawala  Mkoa wa Mwanza amesema kutokana na umuhimu wa Ujenzi wa jengo hilo Ofisi yake itasaidia kutoa ushauri wa namna ya kufanikisha kwa kufanya mapitio kwenye bajeti inayoendelea kutekelezwa na Halmashauri hizo mbili na kwa kuangalia vipaumbele Ujenzi huo utawezekana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.